Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 23:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yawe ameunyoosha mukono wake juu ya bahari amezitetemesha falme; ametoa amri kuharibu makimbilio ya Kanana.

Gade chapit la Kopi




Isaya 23:11
30 Referans Kwoze  

Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.


Akawaambia wachuuzi wa njiwa: “Muondoshe vile vitu hapa. Musifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”


Kisha akawafundisha maneno haya: “Imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi kwa mataifa yote.’ Lakini ninyi mumeigeuza kuwa nafasi ya kukutania ya wanyanganyi!”


Kila chungu katika Yerusalema na inchi ya Yuda kitatolewa kwa Yawe wa majeshi, kusudi wote wanaotoa sadaka waweze kuvitumia kwa kupikia nyama ya sadaka. Wakati ule, hakutakuwa muchuuzi yeyote katika hekalu la Yawe wa majeshi.


Nitayatikisa mataifa yote na mali zao zote zitaletwa humu, nami nitaifanya nyumba hii kuwa yenye utukufu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Yawe ameamuru hivi juu ya Ninawe: Hautapata wazao kwa kulidumisha jina lako. Sanamu zako za kuchonga na za chuma chenye kuyeyushwa, nitazivunjavunja katika nyumba za miungu yako. Mimi nitakuchimbia kaburi lako, maana wewe haufai kwa kitu chochote.


Niliyafanya mataifa yatetemeke kwa sauti ya kuanguka kwake, wakati nilipouangusha chini katika kuzimu pamoja na wale wanaoshuka ndani ya shimo kwa wafu. Nayo miti yote ya Edeni, miti mizuri na ya pekee ya Lebanoni ambayo ilimwangiliwa maji, ilifarijiwa huko chini kwa wafu.


Farasi wa mufalme Nebukadneza ni wengi na mavumbi watakayorusha juu yatakufunika. Kuta zako zitatetemeka kwa mushindo wa waaskari wapanda-farasi na magari ya vita na ya mizigo wakati atakapoingia kwenye milango yako kama watu wanavyoingia katika muji kupitia pahali palipobomolewa.


Lakini utaweza kutulia namna gani, ikiwa ni Yawe ameupa kazi? Ameuamuru ushambulie muji wa Askeloni na watu wanaoishi kandokando ya bahari.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


walisafiri katika bahari nyingi. Mapato yenu yalikuwa ngano ya Misri, mukaweza kufanya biashara na mataifa.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Ukuwe kikingio changu cha kukimbilia, kimbilio lenye nguvu la kuniokoa, kwa maana wewe ni kikingio na kimbilio langu.


Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui.


akasema: “Kanana alaaniwe! Atakuwa mutumwa wa watumwa kwa wandugu zake.”


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nitazitetemesha mbingu nayo inchi itatikisika katika misingi yake kwa sababu ya kasirani ya Yawe wa majeshi, siku ile ya hasira yangu kali.


Huu ndio uamuzi wa Yawe juu ya dunia yote; hii ndiyo azabu atakayotoa juu ya mataifa yote.


Maji ya muto Nili yatakaushwa, nao utakauka kabisa.


Mulime sasa udongo wenu, enyi wakaaji wa Tarsisi; maana hamuna tena kivuko kwa ajili ya mashua kubwa.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Wataziharibu kuta zako na kuibomoa minara yako. Nitafagia kabisa udongo wako na kukufanya kuwa kama jiwe tupu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite