Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ndiyo maana ninawaambia ninyi: musijali chochote juu yangu, muniache nilie machozi ya uchungu. Musijisumbue kunifariji kwa ajili ya kuangamizwa kwa watu wangu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 22:4
20 Referans Kwoze  

Heri ningepata kibanda cha wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kujiendea. Wote ni wazinzi, ni kundi la watu waasi.


“Sauti inasikilika toka Rama, kilio na malalamiko mengi. Ni Rakeli anayewalilia watoto wake, naye hataki kufarijiwa, kwa maana hawako tena.”


Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza; nitatembea uchi na bila viatu. Nitaomboleza na kulia kama mbweha, nitasikitika na kulia kama mbuni.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Ninamulilia Mungu kwa sauti. Kwa sauti ninamulilia Mungu, anisikie.


Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,


naye Petro akakumbuka maneno yale Yesu aliyomwambia kwamba mbele jogoo hajawika, atakuwa amemukana mara tatu. Basi akatoka inje, akalia kwa uchungu sana.


Huzuni yangu haiwezi kutulizwa, moyo wangu unaugua ndani yangu.


Yawe anasema: Muvae magunia, enyi watu wangu na kugaagaa katika majivu. Muomboleze kwa uchungu, kama mutu anayemulilia mwana wake wa pekee, maana mwangamizaji atakuja, na kuwashambulia kwa rafla.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Muangalie, washujaa wao wanalia, wajumbe wa amani wanaomboleza.


Wanapita katika njia wakivaa magunia. Kwenye paa za nyumba na viwanja vya muji watu wanalia na kukauka kwa machozi.


Kilio hiki kinasikilika Sayuni: Tumeangamia kabisa! Tumefezeheshwa kabisa, kwa maana sherti tuiache inchi yetu, nazo nyumba zetu zibomolewe!


Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.


Watajinyoa vichwa kwa ajili yako na kuvaa gunia. Watalia kwa uchungu wa moyo juu yako.


Mordekayi alipojua yote yaliyotukia, akapasua nguo zake, akavaa nguo ya gunia, na kujitia majivu. Kisha, akapita katikati ya muji akilia kwa sauti ya uchungu.


Nawe mwanadamu, ujikunje kama mutu aliyekata tamaa, uomboleze mbele yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite