Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 22:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Lakini ninyi mukafurahi na kusherehekea. Mulichinja ngombe na kondoo, mukakula nyama na kunywa divai. Ninyi mulisema: Acha tukule na kunywa maana kesho tutakufa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 22:13
16 Referans Kwoze  

Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Ikiwa ni kwa nia ya kimutu, nimepigana na nyama wakali wa pori katika Efeso, jambo lile limenifalia nini? Kama wafu hawafufuki, basi: “Tukule na tukunywe, kwa maana kesho tutakufa.”


Mumeishi katika utajiri na kujifurahisha katika maisha yenu katika dunia. Mumejinenepesha kwa kuwa tayari kwa siku ya kuchinjwa.


Ole kwao wanaokuwa wafundi wa kunywa divai, wanaokuwa hodari sana wa kuchanganya vinywaji vya kulewesha.


Katika karamu zao, hapakosekani vinubi, zeze, ngoma, filimbi na divai. Lakini hawajali matendo ya Yawe, wala kutambua kazi za mikono yake.


Ole kwao wanaoamuka asubui mapema wapate kukimbilia kinywaji cha kulewesha; wanaokesha hata usiku, mpaka divai iwaleweshe!


Lakini waovu hata wakipewa rehema, hawawezi kujifunza kutenda haki. Hata katika inchi ya usawa, wao bado wanatenda maovu, wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.


Ole kwako Yerusalema, mazabahu ya Mungu, muji ambamo Daudi alipiga kambi yake! Miaka inakuja na kupita, na sikukuu zako zinaendelea kufanyika;


Sasa, basi, sikiliza, ewe mupenda raha, wewe unayezani kuwa katika usalama, na kujisemesha: Mimi ndiye. Hakuna mwingine isipokuwa mimi. Sitakuwa mujane hata kidogo, wala sitakufiwa na watoto wangu.


Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite