Isaya 21:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.
Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.
Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.
Adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosira. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.
Kwa hiyo ninalia pamoja na Yaweri kwa ajili ya mizabibu ya Sibuma. Machozi yananitoka kwa ajili yenu, enyi miji ya Hesiboni na Eleale; maana vigelegele vya mavuno ya matunda na ya ngano vimetoweka.
Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.
Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.
Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.