Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 21:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.

Gade chapit la Kopi




Isaya 21:3
17 Referans Kwoze  

Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.


Kama vile mama mwenye mimba anayezaa analia na kugaagaa kwa uchungu, ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Yawe.


Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa; wakashikwa na hofu na kukimbia.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Miji yake itatekwa, kuta zake vilevile. Siku hiyo mioyo ya waaskari wa Moabu itakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Hivyo, nafsi yangu inalilia Moabu kama kinubi, na moyo wangu kwa ajili ya muji wa Kiri-Heresi.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Mufalme wa Babeli amesikia habari zao. Kwa hiyo, mikono yake ikaregea. Ameshikwa na huzuni na uchungu, kama mama anayezaa.


Adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosira. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Kwa hiyo ninalia pamoja na Yaweri kwa ajili ya mizabibu ya Sibuma. Machozi yananitoka kwa ajili yenu, enyi miji ya Hesiboni na Eleale; maana vigelegele vya mavuno ya matunda na ya ngano vimetoweka.


Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.


Mioyo yenu itajaa woga wa kila kitu mutakachoona. Asubui mutasema ‘Heri ingekuwa magaribi’; magaribi itakapofika mutasema ‘Heri ingekuwa asubui’.


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Uchungu, uchungu! Ninagaagaa kwa uchungu! Moyo wangu unapigapiga vibaya. Wala siwezi kukaa kimya. Maana ninaogopa mulio wa baragumu, ninasikia kelele la vita.


Waisraeli wanasema: Tumesikia habari zao. Kwa hiyo mikono yetu imeregea; tumeshikwa na huzuni na uchungu, kama mwanamuke anayezaa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite