Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 21:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.

Gade chapit la Kopi




Isaya 21:2
44 Referans Kwoze  

Yawe akamutolea nabii Yeremia ujumbe huu juu ya Elamu, kwa mwanzo wa utawala wa Zedekia, mufalme wa Yuda.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi.


Ee Mungu, umetutupilia na kutuponda, umewaka hasira. Tafazali uturudishie nguvu.


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


PERESI: ufalme wako umegawanywa kati ya Wamedi na Wapersi.


Yule kondoo dume uliyemwona mwenye pembe mbili, ni wafalme wa Media na Persia.


Uwaazibu kwa ajili ya uovu wao wote. Uwatendee kama ulivyonitendea mimi, kwa sababu ya makosa yangu yote. Ninaugua sana kwa maumivu na moyo wangu unazimia.


Ingawa Babeli ungepanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha kuta zake ndefu, waangamizaji watakuja kutoka kwangu kwa kuuharibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Lakini mimi, Mukombozi wao ni mwenye nguvu. Yawe wa majeshi ndilo jina langu. Hakika nitatetea maneno yao kusudi nilete amani katika inchi yao, lakini taabu kwa wakaaji wa Babeli.


Enyi wafundi wote wapiga mishale, mujipange kwa kuzunguka muji wa Babeli kwa vita; mupige mishale, musiache mushale hata mumoja, maana umenikosea mimi Yawe.


Wewe ulisema: Ole wangu! Yawe ameongezea uchungu juu ya maumivu yangu. Nimechoka na kulalamika, wala siwezi kupumzika.


Waliochoka nitawachangamusha, na waregevu nitawapa nguvu.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Niliwakasirikia watu wangu, Israeli, nikawafanya watu wangu kuwa wanaharamu. Niliwatia katika mikono yako, nawe haukuwaonea huruma; na wazee uliwabebesha nira nzito sana.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Majeshi ya Elamu, pinde na mishale katika mikono, walikuja wamepanda farasi na magari ya vita; nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.


Kuwa na akili kunaleta ukubali, lakini njia ya waovu ni ya taabu.


Kilio cha hao wafungwa kikufikie; kwa nguvu yako kubwa uwaokoe waliohukumiwa kufa.


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Yawe aamue kati yangu na wewe. Naye ndiye akulipize kisasi lakini mimi sitanyoosha mukono wangu juu yako hata kidogo.


Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Usimwache anayekutumainia kupata haya; lakini wafezeheke wote wanaokuasi kwa makusudi.


Ninapowaona waasi hao ninachukizwa sana, kwa sababu hawashiki amri zako.


Basi, mufalme Belsasari akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakubwa wake wakakuwa na wasiwasi.


Wana wa Semu walikuwa Elamu, Asuri, Aripakisadi, Ludi na Aramu.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


utaimba wimbo huu wa kumuchekelea mufalme wa Babeli: Jinsi gani mutesaji alikomeshwa! Ukali wake umekomeshwa!


Sasa dunia yote ina utulivu na amani, kila mutu anaimba kwa furaha.


wafalme wote wa Simuri, Elamu na Medi;


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitavunja upinde wa watu wa Elamu unaokuwa musingi wa nguvu zao.


Katika maono haya, nilijikuta niko Susani, muji mukubwa wa jimbo la Elamu. Nilikuwa nimesimama kando ya muto Ulayi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite