Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 21:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nami mulinzi nikajibu: Asubui inakuja, vilevile usiku; ukitaka kuuliza, uliza tu; kwenda urudi tena.

Gade chapit la Kopi




Isaya 21:12
16 Referans Kwoze  

Wakati umetimia, ile siku imekaribia. Mununuzi asifurahi wala muchuuzi asiomboleze; kwa sababu kasirani yangu itawaangukia watu wote.


Muangalie, siku ile inakuja! Maangamizi yenu yamekuja. Ubaya uko kila pahali na kiburi kimepanda sana.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa, lakini mbele ya asubui yametoweka! Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata na kutunyanganya mali yetu.


Muwaue waaskari wake hodari; muache washukie kwenye machinjo. Ole kwao, maana siku yao imetimia, wakati wao wa kuazibiwa umefika!


Ujumbe wa Mungu juu ya Duma. Ninasikia mutu ananiita kutoka Seiri: Mulinzi, nini kipya leo usiku? Kuna kipya chochote leo usiku?


Ujumbe wa Mungu juu ya Arabia. Enyi makundi ya wasafiri ya Dedani, mupige kambi leo usiku katika pori za Arabia.


Haya ni maono ya Obadia. Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya taifa la Edomu. Tumepata habari kutoka kwa Yawe; mujumbe ametumwa kati ya mataifa: Musimame! Tuende tupigane na taifa la Edomu!


Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite