Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 20:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi, mufalme wa Asuria atawapeleka Wamisri na Wakushi kuwa wafungwa, wakubwa kama vile wadogo. Watapelekwa, nao watatembea uchi na bila viatu, matako wazi. Misri ipate haya!

Gade chapit la Kopi




Isaya 20:4
18 Referans Kwoze  

Nitawatia Wamisri katika mikono ya bwana mukali, mufalme mukali ambaye atawatawala. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Nitapandisha kanzu yako mpaka kwenye kichwa hata uchi wako upate kuonekana wazi.


Nawe utajiuliza hivi katika moyo wako: Kwa nini mambo haya yamenipata? Sawa! Ikiwa kanzu yako imepandishwa, na kutendewa kwa kinguvu, hayo ni matokeo ya makosa yako mengi sana.


Kwa hiyo ninakushauria kununua kwangu zahabu iliyosafishwa kwa moto, kusudi upate kuwa tajiri. Vilevile ununue nguo nyeupe, upate kuvaa na kufunika uchi wako unaokuletea haya. Tena ununue dawa ya kutia ndani ya macho yako, kusudi upate kuona.


Enyi wakaaji wa Safiri, muende mukiwa uchi na wenye haya. Wakaaji wa Zanana musitoke inje ya muji wenu. Watu wa Beti-Ezeli wanalia; musaada wao kwenu umeondolewa.


Huko Tapanesi muchana utakuwa giza wakati nitakapovunja mamlaka ya Misri na kiburi chake kikubwa kitakapokomeshwa. Wingu litaifunika inchi ya Misri na watu wake watakamatwa mateka.


Nitawatia katika mikono ya wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao, ni kusema Nebukadneza mufalme wa Babeli na wakubwa wake. Kisha, inchi ya Misri itakaliwa na watu kama ilivyokuwa hapo zamani. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watu watauona uchi wako; wataona haya yako. Mimi nitalipiza kisasi, wala sitamuhurumia mutu yeyote.


Basi, mimi Yawe nitawaazibu; nitawanyoa nywele hao wanawake wa Sayuni, na kuwavua nguo za kufunika uchi wao.


Basi, Hanuni akawakamata wajumbe wale wa Daudi, akanyoa kila mumoja ngambo moja ya ndevu zake, akapasua nguo zao katikati mpaka kwenye matako, kisha akawaacha waende zao.


Utwae mawe ya kusagia, usage unga kama mutumwa! Vua kitambaa chako, pandisha kanzu yako! Onyesha miguu yako kwa kuvuka mito.


Enyi wakaaji wa Misri, mujitayarishe na mizigo kwenda katika uhamisho! Maana muji wa Nofi utaharibiwa kabisa, utakuwa mabomoko yasiyokaliwa na watu.


Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.


Hata hivyo, ulikamatwa mateka, watu wake wakapelekwa katika uhamisho. Hata watoto wake walipondwapondwa katika maingilio ya kila barabara; watu wake wenye heshima waligawanywa kwa kuwapigia kura, wakubwa wake wote walifungwa minyororo.


Nanyi watu wa Kushi vilevile mutauawa kwa upanga.


Basi Hanuni aliwatwaa wajumbe wale wa Daudi, akawanyoa ndevu na kupasua nguo zao katikati mpaka kwenye matako, kisha akawaacha waende zao,


Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi. Habadilishi masemi yake; lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.


Wamisri ni wanadamu tu wala si miungu; farasi wao nao ni nyama tu, si roho. Yawe akiunyoosha mukono wake, taifa linalotoa musaada litajikwaa, na lile linalosaidiwa litaanguka; yote mawili yataangamia pamoja.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite