Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 20:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe akasema: Mutumishi wangu Isaya amekuwa akitembea uchi na bila viatu kwa muda wa miaka mitatu sasa, kama kitambulisho juu ya inchi za Misri na Kushi.

Gade chapit la Kopi




Isaya 20:3
16 Referans Kwoze  

Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Halafu mufalme alipata habari kwamba Tiraka mufalme wa Etiopia anakuja kupigana naye. Akatuma wajumbe kwa Hezekia, akisema:


Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.


Nawe utwae bamba la chuma. Ulisimamishe likuwe kama ukuta wa chuma kati yako na muji. Kisha utaelekezea muji huo uso wako nao utashambuliwa na utaushambulia. Hiki kitakuwa kitambulisho kwa taifa la Waisraeli.


Wakiwa wanakuona, ujibebeshe muzigo wako kwenye mabega na kuondoka wakati wa giza. Funika uso wako usiweze kuona unakwenda wapi. Ndivyo ninavyokufanya kuwa kitambulisho kwa Waisraeli.


Yawe anasema hivi: Wote wanaounga Misri mukono wataangamia, mashujaa wake wenye utukufu wataangamizwa, tangu Migidoli mpaka Sewene watu watauawa katika vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


Nitawatia Wamisri katika mikono ya bwana mukali, mufalme mukali ambaye atawatawala. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Yawe aliniambia hivi: Kwenda ununue mukaba na kuuvaa katika kiuno; lakini usiutie ndani ya maji.


Yawe akaniambia tena: Wewe mwanadamu, twaa tofali, uliweke mbele yako na uchape juu yake muji, kama wa Yerusalema.


Vita itakuja katika inchi ya Misri, na wasiwasi utakuwa katika inchi ya Etiopia, wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa, mali zao zitakaponyanganywa, na misingi ya miji yao kubomolewa.


Nanyi watu wa Kushi vilevile mutauawa kwa upanga.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite