Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 2:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Muingie katika mapango chini ya mawe, katika mashimo ndani ya udongo, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.

Gade chapit la Kopi




Isaya 2:19
41 Referans Kwoze  

Muingie chini ya jiwe, mujifiche katika mavumbi, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake.


Wakati ule watu wataanza kuiambia milima ‘Mutuangukie’, navyo vilima ‘Mutufunike!’


Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!


Nao wataingia katika mapango chini ya mawe na kwenye nyufa za mawe, kwa kuepuka kitisho cha Yawe, mbali na mwangaza wa utukufu wake, atakapokuja kuogopesha dunia.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Katika wakati ule sauti yake ilitetemesha dunia, lakini sasa ametuahidi hivi: “Nitatetemesha dunia mara moja tena, wala si dunia tu, lakini mbingu vilevile.”


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kisha muda kidogo nitazitikisa mbingu na dunia, bahari na inchi kavu.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi na tetemeko kubwa la inchi lisilotokea bado tangia watu walipoanza kuishi katika dunia. Kweli tetemeko lile lilikuwa kubwa sana!


Na saa ile ile, kukatokea tetemeko kubwa la inchi, na sehemu moja ya kumi ya muji ikabomoka, na watu elfu saba wakakufa katika tetemeko lile. Watu waliobaki wakashikwa na hofu, nao wakamutukuza Mungu wa mbinguni.


Na kwa muda ule, watu watatafuta kifo, lakini hakitawapata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.


Dunia haikustahili kuwa na watu kama hawa! Walitangatanga katika jangwa na katika milima, wakiishi katika mapango na mashimo ndani ya udongo.


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


Watatambaa katika mavumbi kama nyoka, kama viumbe vinavyotambaa. Watatoka katika makimbilio yao wakitetemeka na kujaa hofu. Watakugeukia Yawe, Mungu wetu, kwa hofu, wataogopa kwa sababu yako.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.


basi, adui anifuatilie na kunikamata, akomeshe maisha yangu na kuuzika uzima wangu ndani ya mavumbi.


Basi, wakajitokeza kusudi Wafilistini wawaone. Wafilistini walipowaona wakasema: “Muangalie wale Waebrania wanatoka kwenye mashimo walimokuwa wamejificha.”


Waisraeli walipoona wako katika taabu (maana walikuwa wanashambuliwa vikali), walianza kujificha. Wengine walijificha katika mapango, wengine ndani ya mashimo, wengine kwenye mawe makubwa, wengine kwenye makaburi na wengine kwenye visima.


Yeye anaitikisa dunia kutoka pahali pake, na nguzo zake zinatetemeka.


Watakuja makundi kwa makundi na kuyajaza mabonde yenye miinuko, mapango ndani ya mawe, miiba, vichaka vyote na mashamba yote ya kukulishia nyama.


Nitazitetemesha mbingu nayo inchi itatikisika katika misingi yake kwa sababu ya kasirani ya Yawe wa majeshi, siku ile ya hasira yangu kali.


Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake.


Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.


Dunia inavunjikavunjika, inapasuka na kutikiswatikiswa.


Yawe anasema hivi: Sasa mimi nitasimama; sasa nitajiweka tayari; sasa mimi nitatukuzwa.


Kelele la waaskari wapanda-farasi na la wapiga mishale litakaposikilika, watu wote watakimbia. Wamoja wao watakimbilia katika vichaka, wengine watajificha katikati ya mawe. Kila muji utaachwa tupu; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Enyi wenyeji wa Moabu, mutoke katika miji, muende kukaa chini ya mawe! Muige jinsi njiwa anavyojenga chicha chini ya jiwe.


Uwaambie hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kama vile ninavyoishi, hao wanaokaa katika miji hiyo inayokuwa mabomoko, wataagamia kwa upanga; anayekuwa katika vijiji nitamutoa akuliwe na nyama wakali; na wale wanaokuwa kwa milima na ndani ya mapango watakufa kwa ugonjwa mukali.


Ninawe, nawe vilevile utalewa; utamukimbia adui na kujaribu kujificha.


Nitayatikisa mataifa yote na mali zao zote zitaletwa humu, nami nitaifanya nyumba hii kuwa yenye utukufu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Wageni walivunjika moyo; wakakuja kutoka makimbilio yao wakitetemeka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite