8 Wavuvi wataomboleza, wote wanaotumia ndoana watalalamika, wote wanaotega nyavu humo watavunjika moyo.
Wakaldea wanawavua watu kwa ndoana, wanawakokotea inje kwa nyavu zao, wanawakusanya wote katika wavu wao, kisha wanafurahi na kushangilia.
Wavuvi watasimama kandokando ya bahari, na nafasi toka Engedi mpaka Eni-Eglaimu itakuwa ya kuanikia nyavu. Kutakuwa aina nyingi za samaki kama zinavyokuwa katika bahari ya Mediteranea.
Tunakumbuka, samaki tuliokula katika Misri bila malipo, maboga, matikiti, mboga, vitunguu na vitunguu sumu!
Samaki wakakufa, muto ukanuka vibaya sana hata Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Inchi nzima ikajaa damu.
‘Tuliwapigia ngoma, lakini hamukucheza! Tuliimba wimbo wa kilio, lakini hamukulia!’
Hawataacha hata kidogo kuvuta upinde wao? Wataendelea tu kuwanasa watu, na kuyaangamiza mataifa bila huruma?