Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 19:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Yawe wa majeshi ameunyoosha mukono wake juu yao.

Gade chapit la Kopi




Isaya 19:16
18 Referans Kwoze  

Angalia, waaskari wako ni wanawake tu. Milango ya inchi yako ni wazi mbele ya waadui zako; moto umeteketeza kabisa vifungio vyake.


Waaskari wa Babeli wameshindwa kupigana, wamebaki katika makimbilio yao; nguvu zao zimewaishia, wamekuwa kama wanawake. Nyumba za Babeli zimechomwa kwa moto, milango yake ya chuma imevunjwa.


Upanga ukuwe juu ya farasi wake na magari yake, juu ya majeshi yake yote ya mushahara, kusudi wakuwe sawa na wanawake! Upanga ukuwe juu ya hazina zake zote kusudi zinyanganywe.


Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.


Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.


Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba, anainua mukono wake kwa mulima Sayuni, kilima cha Yerusalema.


Kuanguka katika mikono ya Mungu Mwenye Uzima ni jambo la kuogopa sana!


Watu wenu elfu moja watamukimbia askari mumoja adui; na waaskari watano waadui watawakimbiza ninyi wote. Kwa mwisho, watakaobaki, watakuwa kama muti wa bendera kwa mulima, kama kitambulisho kinachokuwa juu ya kilima.


Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa; wakashikwa na hofu na kukimbia.


Sababu ya hii nilikuwa kwenu katika hali ya uzaifu na woga, mwenye kutetemeka sana.


Basi, kwa sababu tunajua kwamba ni lazima kumwogopa Bwana, ndiyo maana tunajitoa kuwavuta watu kwake. Mungu anatujua waziwazi nami ninatumaini kwamba ninyi wenyewe munatujua waziwazi vilevile.


Mungu anasema: Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti, muwapigie waaskari kelele, muwapepee watu kwa mukono, mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.


Kutakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri, kilio ambacho hakijapata kutokea, wala hakitatokea tena.


Ewe muji wa Temani, mashujaa wako wataogopa na kila mutu juu ya mulima wa wazao wa Esau.


Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.


Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite