Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 19:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Wakubwa wa muji wa Soani ni wapumbafu kabisa, washauri wa Mufalme wa Misri wanatoa shauri la kijinga! Kila mumoja anaweza namna gani kumwambia Mufalme wa Misri: Mimi ni wa uzao wa wenye hekima, wa uzao wa wafalme wa zamani!

Gade chapit la Kopi




Isaya 19:11
31 Referans Kwoze  

Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).


Musa akafundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri, akakuwa mwenye uwezo sana katika masemi yake na matendo yake.


Maana ingawa wakubwa wao wamefika Soani, na wajumbe wao mpaka katika muji wa Hamesi,


alipotenda maajabu katika inchi ya Misri, na miujiza katika mbuga za Soani!


Alifanya maajabu mbele ya babu zao, katika mbuga za Soani kule Misri.


Muji wa Patro nitaufanya kuwa tupu, muji wa Soani nitauteketeza kwa moto, nitauazibu muji wa No.


Watapata hasara kwa mufululizo; nazo habari mbaya zitafuatana. Watamwomba nabii awatabirie. Makuhani hawatakuwa na sheria yoyote; na wazee watakosa shauri la kuwapatia.


Juu ya Edomu, Yawe wa majeshi anasema hivi: Hakuna tena hekima katika muji wa Temani? Wenye hekima wao hawana shauri tena? Hekima imetoweka kabisa?


Nami Yeremia nikasema: Wachungaji wamekuwa wajinga, hawakuuliza shauri kwa Yawe; kwa sababu hiyo, hawakufanikiwa, na kondoo wao wote wamesambaa.


Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.


Mimi ninavuruga maono ya manabii wa uongo na ninapoteza akili za waaguzi. Mimi ninayapinga maneno ya wenye hekima na kufanya elimu yao kuwa upumbafu.


Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.


Lakini wakubwa wa Soani ni wapumbafu, wakubwa wa Nofi wamedanganyika. Hao wanaokuwa musingi wa makabila yao wamelipotosha taifa la Misri.


Nitawaondolea Wamisri uhodari wao. Nitaivuruga mipango yao. Watatafuta shauri kwa sanamu na mizimu, wachawi, mizuka na pepo.


Mimi ni mupumbafu sana, wala si mutu; sina akili ya mwanadamu.


Matendo yako, ee Yawe, ni makubwa sana! Mawazo yako hayatambulikani!


nilikuwa mupumbafu na mujinga, nilikuwa kama nyama mbele yako.


Yawe anavunja mipango ya mataifa, na anabadilisha mawazo yao.


Anawatembeza washauri miguu wazi, anawafanya waamuzi kuwa wapumbafu.


Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?


Naye Mufalme wa Misri, mumupange jina hili: Mwenye domo ya bure!


Ulikuwa na kiburi kwa sababu ya uzuri wako. Uliharibu hekima yako kwa sababu ya utukufu wako. Nilikutupa chini kwenye udongo, nikakufanya kuwa kitisho kwa wafalme.


Washirika wenzenu wamewadanganya, wamewafukuza toka katika inchi yenu. Watu muliopatana nao wamewashinda katika vita. Warafiki wa kutegemewa ndio waliokutegea mitego, nawe haukuelewa yaliyokuwa yanatendeka.


Kisha mufalme wa Misri akamwita Musa na Haruni, akawaambia: “Musihi Yawe, kusudi aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli wajiendee na kutoa sadaka kwa Yawe.”


Wachawi wa Misri, kwa uchawi wao, wakajaribu kuyageuza mavumbi yakuwe chawa, lakini hawakuweza. Chawa wale wakaenea juu ya watu na nyama.


Hekima ya Solomono iliipita hekima ya watu wa mashariki na iliishinda hekima ya watu wa Misri.


Mimi Yawe ninakuuliza hivi: Siku hiyo, sitawaangamiza wenye hekima kutoka Edomu na wenye maarifa kutoka mulima wa wazao wa Esau?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite