Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 19:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.

Gade chapit la Kopi




Isaya 19:1
36 Referans Kwoze  

“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


Mara tu tuliposikia mambo hayo, tukavunjika moyo kabisa kwa sababu yenu, tukaishiwa nguvu kabisa. Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu juu mbinguni na chini katika dunia!


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaharibu sanamu za miungu, na kukomesha miungu ya uongo ya muji wa Nofi. Hakutakuwa mukubwa tena huko Misri. Nitasababisha hofu itawale katika inchi ya Misri.


Nitamwazibu mungu Beli huko Babeli, nitamutapikisha kile alichomeza. Mataifa hayatamwendea tena kwa wingi. Ukuta wa Babeli umebomoka.


Mutangaze kati ya mataifa, munyanyue bendera na kutangaza, musifiche jambo lolote. Museme: Babeli umetekwa, mungu Beli amepatishwa haya. Merodaki amefazaishwa; sanamu zake zimefezeheshwa, miungu yake imefazaishwa.


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


umejenga makao yako katika mbingu juu ya maji. Umeyafanya mawingu kuwa gari lako nawe unatembea katika anga.


Musa akamalizia kwa kusema: “Ee Israeli, hakuna anayekuwa kama Mungu wako, yeye anayeruka toka mbinguni kuja kukusaidia, anapita juu katika anga katika utukufu wake.


Ikiwa Wamisri watakataa kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda, basi, Yawe atawapiga kwa ugonjwa uleule atakaowapiga nao mataifa yote yanayokataa kushiriki kwa sikukuu hiyo.


Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.


Mufalme wa Misri, wasimamizi wake na wakubwa wa serikali yake pamoja na watu wake wote;


Angalia, wanakuja: waaskari wapanda-farasi wawiliwawili. Wanasema: Babeli umeanguka! Umeanguka! Sanamu zote za miungu yake zimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!


Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Yawe wa majeshi ameunyoosha mukono wake juu yao.


Kwa hiyo mikono ya kila mutu itaregea, kila mutu atavunjika moyo.


Upendezwe na hayo mashairi yangu, ee Yawe, maana wewe ndiye furaha yangu.


Lakini watu wa haki wanafurahi Mungu anapokuja, wanashangilia na kuimba kwa furaha.


Wakamwambia: “Hakika Yawe ameitia inchi yote katika mikono yetu. Tena wakaaji wa inchi hiyo wametetemeka kwa sababu yetu.”


akawaambia: “Mimi ninajua kwamba Yawe amewapa inchi hii; tumepatwa na hofu juu yenu na wakaaji wote wa inchi hii wanatetemeka kwa sababu yenu.


Moshi ulifuka kutoka katika pua lake, moto wenye kuteketeza ukatoka katika kinywa chake, makaa ya moto yakatokea.


Angalia! Adui anakuja akivuma kama mawingu. Magari yake ya vita ni kama zoruba, nao farasi wake wa vita wanaruka mbio kuliko tai. Ole kwetu! Tumeangamia!


Kwa nini munanichochea nikasirike kwa kuabudu sanamu mulizojitengenezea wenyewe na kuifukizia ubani miungu mingine katika inchi ya Misri ambamo mumekuja kuishi? Munataka kuangamizwa na kuwa laana na kuchekelewa mbele ya mataifa yote katika dunia?


Ujumbe wa Mungu juu ya Ninawe. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkosi.


Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.


ambao walikuwa wanazika wazaliwa wao wa kwanza wanaume Yawe aliowaua; maana Yawe alikuwa ameiazibu hata miungu yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite