Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 18:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ole, kwa inchi iliyojaa muvumo wa mabawa, inchi inayokuwa ngambo ya mito ya Kushi!

Gade chapit la Kopi




Isaya 18:1
18 Referans Kwoze  

Kutoka ngambo ya mito ya Kushi watu wangu wanaoniomba, wale ambao wametawanyika, wataniletea sadaka yangu.


Halafu mufalme alipata habari kwamba Tiraka mufalme wa Etiopia anakuja kupigana naye. Akatuma wajumbe kwa Hezekia, akisema:


Nanyi watu wa Kushi vilevile mutauawa kwa upanga.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha Waetiopia wanaojizania kuwa na usalama. Watatetemeka siku Misri itakapoangamia. Kweli! Kweli siku hiyo inakuja!


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.


Ninakukumbuka ninapokuwa katika kitanda, ninafikiri juu yako usiku kucha,


Wewe ndiwe kimbilio langu, boma langu lenye nguvu la kukimbilia waadui.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.


Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama vilindi vya bahari. Wewe, ee Yawe, unawalinda wanadamu na nyama.


Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche chini ya kivuli cha mabawa yako,


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


Halafu mufalme alipata habari kwamba Tiraka mufalme wa Etiopia anakuja kupigana naye. Akatuma wajumbe kwa Hezekia, akisema:


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite