Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 16:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Kama ndege wanavyohangaika na kurukaruka, wakiwa wamefukuzwa kutoka chicha zao, ndivyo wabinti wa Moabu wanavyokuwa kwenye vivuko vya Arnoni.

Gade chapit la Kopi




Isaya 16:2
14 Referans Kwoze  

Mutu aliyepotea mbali na kwake ni kama ndege aliyepotea mbali na chicha yake.


Kisha wakasafiri wakipitia katika jangwa kuzunguka inchi ya Edomu na Moabu mpaka walipofika upande wa mashariki wa Moabu, wakapiga kambi ngambo ya muto Arnoni. Lakini hawakuingia katika eneo la Moabu. Muto Arnoni ndio uliokuwa mupaka wa Moabu.


Moabu imepatishwa haya maana imevunjika. Muomboleze na kuililia. Mutangaze kandokando ya muto Arnoni, kwamba Moabu imeharibika kabisa.


Kama swala anayewindwa, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji, kila mumoja atajiunga na watu wake, kila mutu atakimbilia katika inchi yake.


ilikuwa kuanzia Aroeri pembeni ya bonde la Arnoni na muji uliokuwa katika bonde hilo pamoja na inchi yote ya bonde ya Medeba.


“Tulipoitwaa inchi hiyo, nikawapa makabila ya Rubeni na Gadi eneo la kuanzia upande wa kaskazini wa Aroeri karibu na Arnoni na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.


“Wakati huo tukatwaa inchi hiyo ya wale wafalme wawili wa Waamori waliokuwa wanakaa ngambo ya muto Yordani, katikati ya muto Arnoni na mulima Hermoni.


Kuanzia Aroeri, muji unaokuwa kwenye ukingo wa bonde la Arnoni, na ule muji mwingine unaokuwa ndani ya bonde hili mpaka inchi ya Gileadi, hakuna muji wowote ambao hatukuweza kuushinda. Yawe aliitia miji yote katika mikono yetu.


Ole wenu watu wa Moabu! Mumeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemosi! Umewafanya watoto wenu wanaume kuwa wakimbizi, wabinti zako umewaacha watwaliwe mateka mpaka kwa Sihoni, mufalme wa Amori.


Mufalme Mesha wa Moabu alikuwa mufugaji wa kondoo, na kila mwaka alilipa kodi kwa mufalme wa Israeli wana-kondoo elfu mia moja na manyoya ya kondoo wengine elfu mia moja.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Muchimbie Moabu kaburi, maana kuangamia kwake ni hakika; miji yake itakuwa tupu, bila mukaaji hata mumoja.


Ole kwenu watu wa Moabu! Watu wa Kemosi sasa mumeangamizwa, wana wenu wamekamatwa mateka, wabinti zenu wamepelekwa katika utumwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite