Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 15:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Watu wa Diboni wamepanda katika hekalu pahali pa juu kwa kuomboleza, watu wa Moabu wanalia kwa ajili ya Nebo na Medeba; vichwa vyote vimenyolewa upaa, ndevu zao zote zimekatwa kabisa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 15:2
34 Referans Kwoze  

Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;


Wazao wa Haruni wasijinyoe upaa kwa kuomboleza wala wasikate pembe za ndevu zao wala kujichanja chanjo juu ya mwili.


Enyi wenyeji wa Diboni: mushuke kutoka pahali penu pa utukufu, muikae juu ya udongo usiokuwa na maji. Maana mwangamizaji wa Moabu, amefika kuwashambulia; amekwisha haribu kuta zenu.


Kwa pahali pa harufu ya marasi watatoa uvundo; kwa pahali pa mikaba mizuri watatumia kamba; kwa pahali pa nywele nzuri watakuwa na upaa; kwa pahali pa nguo nzuri watavaa magunia; uzuri wao wote utageuka kuwa haya.


Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,


Lakini sasa wazao wao wameangamizwa, kutoka Hesiboni mpaka Diboni, kutoka Nasimu mpaka Nofa, karibu na Medeba.


Watavaa gunia, hofu itawashika, nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.


Kwa hiyo ninaomboleza juu ya Moabu, ninalia kwa ajili ya Wamoabu wote, ninaomboleza juu ya watu wa Kiri-Heresi.


Watu wa Gaza wamenyoa kichwa kwa kuomboleza; muji wa Askeloni umeangamia. Enyi watu muliobaki katika bonde mutajikatakata kwa huzuni mpaka wakati gani?


Munyoe nywele zenu na kuzitupa, enyi wakaaji wa Yerusalema: mufanye maombolezo juu ya vichwa vya milima, maana, mimi Yawe nimewakataa ninyi, nimewatupilia ninyi kizazi kilichosababisha hasira yangu!


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Watu wa Moabu wanapojitokeza kuabudu mungu wao, wanapojichokesha huko juu pahali pa ibada, wanapokwenda pahali pao patakatifu kwa kuomba, hawatakubaliwa.


Sasa Wamoabu wanalia; wote wanaomboleza juu ya inchi yao. Muomboleze kwa ajili ya pigo hilo kubwa, na juu ya maandazi ya zabibu za Kiri-Hareseti.


Wanapita katika njia wakivaa magunia. Kwenye paa za nyumba na viwanja vya muji watu wanalia na kukauka kwa machozi.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


Kisha Yobu akasimama, akapasua nguo yake, akanyoa nywele zake, akajitupa chini na kumwabudu Mungu,


“Ninyi ni watoto wa Yawe, Mungu wenu; musijichanje wala kunyoa nywele upande wa mbele kwa ajili ya mutu aliyekufa.


Nebo na Bali-Meoni (majina ya hiyo miji yalibadilishwa), na Sibuma. Miji waliyoijenga wakaipa majina mengine.


Miji ya Ataroti, Diboni, Yazeri, Nimura, Hesiboni, Eleale, Sebamu, Nebo na Beoni,


Kama mwanaume amepata upaa, yeye ni safi maana ana upaa tu.


Maana moto ulitoka Hesiboni, miali ya moto ilitoka katika muji kwa Sihoni, ukauteketeza muji wa Ari wa Moabu, ukaiangamiza milima ya muto Arnoni.


Basi, Hanuni akawakamata wajumbe wale wa Daudi, akanyoa kila mumoja ngambo moja ya ndevu zake, akapasua nguo zao katikati mpaka kwenye matako, kisha akawaacha waende zao.


Kelele linasikilika juu ya vilima: Waisraeli wanalia na kuomboleza, kwa sababu wamepotoka katika njia zao, wamenisahau mimi Yawe, Mungu wao.


Yawe anasema hivi: Maji yanapanda kutoka kaskazini, nayo yatakuwa muto uliofurika; yataifunika inchi nzima na vyote vinavyokuwa ndani yake, muji na wakaaji na wanaoishi humo. Watu watalia, wakaaji wote wa inchi wataomboleza.


Nami nitamuteketeza kila mutu katika Moabu ambaye anatambikia juu ya vilima na kumufukizia mungu wake ubani. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watajinyoa vichwa kwa ajili yako na kuvaa gunia. Watalia kwa uchungu wa moyo juu yako.


Wewe mwanadamu! Toa unabii useme hivi: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Muomboleze na kusema: Ole kwetu siku ile!


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Basi Hanuni aliwatwaa wajumbe wale wa Daudi, akawanyoa ndevu na kupasua nguo zao katikati mpaka kwenye matako, kisha akawaacha waende zao,


Muomboleze, enyi watu wa Hesiboni, maana muji Ai umeharibika! Mulie, enyi wabinti wa Raba! Muvae magunia, muomboleze na kukimbia huko na huko ndani ya ukuta wenu! Maana mungu Milkomu atapelekwa katika uhamisho, pamoja na makuhani wake na watumishi wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite