Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 15:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Moabu. Muji wa Ari katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku; muji wa Kiri katika inchi ya Moabu umeangamizwa usiku.

Gade chapit la Kopi




Isaya 15:1
20 Referans Kwoze  

Wote pamoja watashambulia Wafilistini wanaokuwa upande wa magaribi, pamoja watawanyanganya watu wanaokaa upande wa mashariki. Watawashinda Waedomu na Wamoabu, nao Waamoni watawatii.


Maana moto ulitoka Hesiboni, miali ya moto ilitoka katika muji kwa Sihoni, ukauteketeza muji wa Ari wa Moabu, ukaiangamiza milima ya muto Arnoni.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


Hivyo, nafsi yangu inalilia Moabu kama kinubi, na moyo wangu kwa ajili ya muji wa Kiri-Heresi.


Sasa Wamoabu wanalia; wote wanaomboleza juu ya inchi yao. Muomboleze kwa ajili ya pigo hilo kubwa, na juu ya maandazi ya zabibu za Kiri-Hareseti.


Mwaka mufalme Ahazi alipokufa, Mungu alitoa ujumbe huu:


Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli:


na kuibomoa miji yao. Kila nafasi walipopita kwenye shamba zuri, kila mutu alilirushia jiwe mpaka kila shamba likajaa mawe; vilevile wakaziziba chemichemi zote za maji na kukata miti yote mizuri. Nyuma ya hayo, kukabaki muji mukubwa wa Kiri-Haraseti peke yake, ambao waaskari wapiga-kombeo waliuzunguka na kuuteka.


‘Leo hii mutauvuka mupaka wa Moabu kwa kupitia inchi ya Ari.


Yawe akaniambia: ‘Usiwasumbue watu wa Moabu, wala usipigane nao maana sitawapa sehemu yoyote ya inchi yao. Lakini eneo hilo la Ari nimewapa hao wazao wa Loti likuwe mali yao.’


Atabomoa pango za miji ya Moabu yenye kuta ndefu na kuiangusha chini ndani ya mavumbi.


Mutaifikia inchi ya Waamoni. Musiwasumbue wala musipigane nao kwa sababu sitawapa sehemu yoyote ya hao wazao wa Amoni ikuwe mali yenu. Hao ni wazao wa Loti, na nimewapa hiyo inchi ikuwe mali yao.’ ”


Watu wa Yuda wanasema hivi: Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, tunajua jinsi alivyojivuna sana; tumesikia juu ya majivuno, kiburi na mazarau yake; lakini majivuno yake hayo ni bure.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite