Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 13:6
39 Referans Kwoze  

Ole kwetu kwa ile siku ya Yawe, siku hiyo ya Yawe inakaribia; inakuja pamoja na maangamizi, kutoka kwa Mungu Mukubwa.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


Ole kwenu ninyi munaoingojea kwa hamu siku ya Yawe! Kwa nini munaitaka sana siku hiyo? Siku hiyo, itakuwa siku ya giza na si ya mwangaza!


Siku ya Yawe inakuja, siku kali, ya kasirani na hasira kali. Itaifanya inchi kuwa uharibifu, itawaangamiza wenye zambi ndani yake.


Watasimama kwa mbali kwa ajili ya kuogopa yale mateso yake, wakisema: “Ole, ole kwako ewe muji Babeli, muji mukubwa na wenye uwezo! Kwa saa moja tu azabu yako imetimia!”


Yawe anaamuru kundi lake kwa sauti; waaskari wake ni wengi sana, wanaomutii hawahesabiki. Siku ya Yawe kweli ni kubwa na ya kutisha sana! Nani atakayeweza kuivumilia?


Kwa rafla Babeli imeanguka na kuvunjikavunjika; muomboleze kwa ajili yake! Mulete dawa kwa kutuliza maumivu yake; labda utaweza kupona.


Maana Yawe yuko na siku ya kulipiza kisasi; mwaka wa kulipiza waadui za Sayuni.


Kweli, siku ya Yawe wa majeshi inakuja juu ya wote wenye kiburi na majivuno, juu ya wote wanaojitukuza,


Basi, munisikilize sasa ninyi watajiri! Mulie na kuomboleza kwa sababu ya taabu itakayowapata.


Ile siku kubwa ya Yawe imekaribia, iko karibu na inakuja mbio. Mulio wa siku ya Yawe ni wa uchungu; hapo, hata shujaa atalia kwa sauti.


Enyi makuhani, muvae magunia kwa kuomboleza, mulie, enyi munaotumika kwenye mazabahu. Muingie katika hekalu muomboleze usiku kucha! Sadaka za chakula na kinywaji zimetoweka katika nyumba ya Mungu.


Enyi walevi, muamuke na kulia; enyi walevi wa divai, mulalamike; zabibu zote za kutengeneza divai mupya zimeharibiwa.


Ulie ewe mulango; ulalamike ewe muji; tetemeka kwa hofu, ewe inchi yote ya Filistia. Maana moshi wa waaskari unakuja kutoka kaskazini, wala hakuna atakayechelewa katika makundi yake.


Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.


Muomboleze, enyi walimaji; mulalamike, enyi watunza mizabibu. Ngano na shayiri zimeharibika, mavuno yote katika shamba yameangamia.


Wakikuuliza hivi: Kwa nini unaomboleza? Utawaambia: Ninaomboleza kwa sababu ya habari zinazokuja. Kila mutu atavunjika moyo, mikono yao yote itaregea; kila mutu anayeishi atazimia na magoti yao yataregea. Habari hizo zinakuja kweli, nazo zinatimia. –Ni Bwana wetu Yawe anayesema hivyo.


Muomboleze, enyi watu wa Hesiboni, maana muji Ai umeharibika! Mulie, enyi wabinti wa Raba! Muvae magunia, muomboleze na kukimbia huko na huko ndani ya ukuta wenu! Maana mungu Milkomu atapelekwa katika uhamisho, pamoja na makuhani wake na watumishi wake.


Watumishi wangu wataimba kwa furaha ndani ya moyo, lakini ninyi mutalia kwa uchungu ndani ya moyo na kupiga kelele kwa uchungu mukubwa ndani ya roho.


Katika hali ya sasa ninapata faida gani kuwaona watu wangu wamepelekwa katika utumwa? –Ni ujumbe wa Yawe. Hao wanaowatawala wanajitapa. Nalo jina langu linaendelea kuzarauliwa kila siku. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ujumbe wa Mungu juu ya Tiro. Muomboleze, enyi mashua makubwa za kutoka Tarsisi. Kivuko na muji wenu vimeharibiwa. Mutapokea habari hizo mutakaporudia kutoka Kipuro.


Muomboleze, enyi wachungaji; mulie na kugaagaa katika majivu, enyi wakubwa wa kundi. Siku za kuchinjwa kwenu na kusambazwa zinakaribia. Mutauawa kama kondoo dume wanene.


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


Maana bado kidogo, nayo hasira yangu itapita na kasirani yangu itawageukia Waasuria.


Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa tingitingi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Yawe amekasirikia mataifa yote, amekasirikia majeshi yao yote. Ameyapangia mwisho wao, ameyatoa yaangamizwe.


Lakini hasara itakupata ambayo hautaweza kujiepusha nayo. Magumu yatakutokea ambayo hautaweza kuyapinga; maangamizi yatakufikia kwa rafla ambayo haujapata kuyaona hata kidogo.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Hawakwenda kulinda sehemu zile za kuta zilizobomoka wala hawajengi kuta mupya kusudi Waisraeli waweze kujilinda wakati wa vita siku ile ambayo mimi Yawe nimeiweka.


Basi, mufalme Belsasari akazidi kuhangaika na rangi yake ikazidi kugeuka, nao wakubwa wake wakakuwa na wasiwasi.


Na hii ndiyo maana yake. MENE: Mungu amehesabu siku za ufalme wako na kuukomesha.


Angalia, siku ya kasirani ya Yawe inakuja. Siku hiyo, enyi watu wa Yerusalema, mali yenu itagawanywa mbele ya macho yenu.


Niliamua kwamba siku ya kulipiza kisasi imefika; wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.


Mupige baragumu kule Sayuni; mupige kelele la kujulisha hatari kule juu ya mulima mutakatifu! Mutetemeke enyi wakaaji wa Yuda, maana siku ya Yawe inakuja, siku hiyo iko karibu!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite