Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 13:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Fisi watalia ndani ya pango zake, mbweha wataonekana ndani ya nyumba zao za raha. Wakati wa Babeli umekaribia, wala siku zake hazitaongezwa.

Gade chapit la Kopi




Isaya 13:22
19 Referans Kwoze  

Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Babeli ni kama uwanja wa kupepetea ngano wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.


Muchanga wa moto katika jangwa utakuwa ziwa la maji, inchi kavu itabubujika vijito. Makao ya imbwa wa pori yatajaa maji; nyasi zitaota na kukomaa kama mianzi.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.


Maono haya yanangoja wakati uliopangwa; ni maono ya ukweli juu ya mwisho. Kama yanaonekana kuchelewa, uyangojee; hakika yatafika, wala hayatachelewa.


Miiba itaota katika pango zake, miiba na michongoma ndani ya kuta zake. Itakuwa makao ya imbwa wa pori, nafasi ya mbuni.


Ni kazi yangu kulipiza kisasi, mimi nitalipiza, wakati miguu yao itakapoteleza; maana siku yao ya hasara imefika mwisho wao uko karibu sana.


Hatujakuasi wewe, wala hatujaiacha njia yako.


Maana nyumba ya kifalme itaachwa ukiwa, muji huo wa watu wengi utahamwa. Mulima na munara wa ulinzi utakuwa mapango milele, punda wa mwitu watapitapita huko kwa furaha, kondoo watapata malisho yao humo.


Nyama wa pori wataniheshimu, mbweha na mbuni, maana nitaweka maji katika mbuga, na kububujisha mito katika jangwa, kwa kuwakunywesha watu wangu niliojichagulia,


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Uharibifu wa Moabu umekaribia, maangamizi yake yanakuja haraka.


Hata mbweha wanatoa maziwa, na kuwanyonyesha watoto wao; lakini watu wangu wamekuwa wabaya, wanafanya kama mbuni katika jangwa.


Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza; nitatembea uchi na bila viatu. Nitaomboleza na kulia kama mbweha, nitasikitika na kulia kama mbuni.


Nitaufanya kuwa makao ya nungunungu, na utakuwa tingitingi ya maji. Nami nitaufagilia mbali kwa ufagio wa maangamizi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Paka wa pori na fisi watakuwa humo, mapepo wataitana humo; sulukutu atatulia humo na kupata nafasi ya kupumzika.


Makundi ya nyama wa kufugwa watalala ndani yake, vilevile kila nyama wa pori. Tai, nyangenyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake, bundi watalia kwenye madirisha yake, vibombobombo watalia kwenye vizingiti, maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite