Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 13:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kama swala anayewindwa, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji, kila mumoja atajiunga na watu wake, kila mutu atakimbilia katika inchi yake.

Gade chapit la Kopi




Isaya 13:14
13 Referans Kwoze  

Halafu, Mikaya akasema: “Niliona watu wote wa Israeli wametawanyika juu ya milima kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Naye Yawe akasema: ‘Watu hawa hawana kiongozi. Basi warudi kila mutu kwake kwa amani.’ ”


Muzuie watu wasipande mbegu Babeli, wala wasivune wakati wa mavuno. Kutokana na upanga wa uharibifu, kila mumoja atawarudilia watu wake, kila mumoja atakimbilia katika inchi yake.


Jua liliposhuka, amri ikatolewa: “Kila mutu arudie kwake! Kila mutu arudie kwake!”


Tulijaribu kuuponyesha Babeli, lakini hauwezi kupona. Muuache, tujiendee, kila mumoja katika inchi yake. Hukumu yake ni kubwa sana inafika mpaka katika mawingu.


Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo, hao uliojishugulisha nao tangu ujana wako. Watatangatanga kila mumoja njia yake; hakuna hata mumoja atakayeweza kukuokoa.


Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.


Yesu alipoona kundi la watu, aliwasikilia huruma, kwa maana walikuwa wamesumbuka na kuregea, kama kondoo wasiokuwa na muchungaji.


Wakati Yesu alipotoka ndani ya chombo, akaona kundi kubwa la watu, akawasikilia huruma, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. Basi akaanza kuwafundisha maneno mengi.


Kwa maana mulikuwa kama kondoo wanaopotea, lakini sasa mumerudi kwa yule anayekuwa muchungaji na mwangalizi wa roho zenu.


Maana wamekimbia mapanga, mapanga yaliyochomolewa, pinde zilizovutwa na ukali wa mapigano.


Hiyo miaka makumi saba itakapopita, nitamwazibu mufalme wa Babeli pamoja na taifa lake. Nitaiangamiza inchi hiyo ya Wababeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitafanya hivyo kwa sababu ya uovu wao na kuifanya inchi ibaki mabomoko hata milele.


Ewe mufalme wa Asuria, wachungaji wako wamelala, waheshimiwa wako wamesinzia. Watu wako wametawanyika kwenye milima, wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite