Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.

Gade chapit la Kopi




Isaya 12:6
40 Referans Kwoze  

Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.


Wanaojua jina lako, wanakutegemea, kwa maana wewe, ee Yawe, hauwatupi wanaokutafuta.


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.


Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.


Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.


Kwenda juu ya mulima murefu, ewe Sayuni, utangaze habari njema. Lalamika kwa nguvu, ewe Yerusalema, utangaze habari njema. Lalamika bila kuogopa. Uambie miji ya Yuda: Muangalie: Mungu wenu!


Nami nitakusifu kwa kinubi, kwa sababu ya uaminifu wako, ee Mungu wangu; nitakuimbia sifa kwa zeze, ewe Mutakatifu wa Israeli.


Ole wenu wakaaji wa inchi za pembeni ya bahari, watu wanaoishi kule Krete! Yawe amesema juu yenu, enyi wakaaji wa Kanana, inchi ya Wafilistini: Mimi nitawaangamiza wala hakutabaki hata mukaaji mumoja!


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


Nitawasukuma watesaji wako wakule miili yao wenyewe; watalewa damu yao wenyewe kama divai. Halafu wanadamu wote watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mwokozi wako, Mukombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.


Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa; watu watasamehewa uovu wao wote.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.


Mimi pamoja na watoto Yawe alionipa ni kitambulisho na mufano katika Israeli kwa jina la Yawe wa majeshi anayekaa kwenye mulima Sayuni.


Yeye anasema: “Hapa ndipo nitakapokaa milele, ndipo makao yangu, maana nimepachagua.


Wewe ndiwe utukufu na nguvu yao; kwa upendo wako tunapata ushindi.


Ewe mulima wa Basani, murefu na wenye vichwa vingi,


Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.


Yawe ni mukubwa katika Sayuni; ametukuzwa kuliko mataifa yote.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Watu wanalalamika, wanaimba kwa shangwe. Kutoka upande wa magaribi, wanatangaza ukubwa wa Yawe,


Utaletewa chakula na watu wa mataifa; wafalme watakupatia chakula bora. Hapo utatambua kwamba mimi Yawe ni Mwokozi wako; mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mukombozi wako.


Ee Yawe, hakuna anayekuwa kama wewe; wewe ni mukubwa na nguvu yako inajulikana.


Wewe ulisema kwamba mataifa hayo mawili, ni kusema inchi ya Yuda na ya Israeli, ni mali yako na kwamba utazirizi! Ulisema hivyo ingawa humo ni makao yangu mimi Yawe.


Nitajulisha jina langu takatifu kwa watu wangu Waisraeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kwamba mimi ni Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Kisha eneo la kabila la Yuda, utatenga eneo lenye urefu wa kilometre kumi na mbili na upana kama huohuo, kutoka kaskazini mpaka kusini, na urefu huohuo kutoka mashariki mpaka magaribi, sawasawa na eneo la kabila lolote. Hapo katikati ya eneo hilo patakuwa hekalu la Mungu.


Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.


Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.


Kambi yenu inapaswa kuwa takatifu kwa sababu Yawe, Mungu wenu anatembea katika kambi yenu kusudi awaokoe na kuwatia waadui zenu katika mikono yenu. Kwa hiyo musimwache aone kitu chochote kisichofaa kati yenu, kama sivyo atawaacha ninyi.


Atukuzwe Yawe katika Sayuni, atukuzwe katika makao yake Yerusalema. Haleluia!


Humo Yawe atatuonyesha ukubwa wake. Kutakuwa mito mikubwa na vijito, lakini mashua za vita hazitapita, wala mashua kubwa kuingia.


Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite