Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 10:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?

Gade chapit la Kopi




Isaya 10:3
40 Referans Kwoze  

Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.


nitafanya nini basi Mungu atakaposimama mbele yangu? Akinichunguza, nitamujibu nini?


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Maana Yawe anakuja kutoka kwake juu, kutoka makao yake huko mbinguni; kuwaazibu wakaaji wa dunia kwa uovu wao. Nayo dunia haitaficha tena wale waliouawa, lakini itaufichua umwagaji wa damu wote.


Wakati huo, wakaaji wa kandokando watasema: Muangalie yaliyowapata watu tuliowategemea na kuwakimbilia kuomba musaada watuokoe na mufalme wa Asuria! Na sasa, sisi tutaweza namna gani kupona?


Yawe ananyunyua bendera kwa kuita taifa la mbali; anawapigia filimbi watu kutoka miisho ya dunia; nao wanakuja mbio na kufika haraka!


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Halafu nabii Isaya alikwenda kwa mufalme Hezekia na kumwuliza: Watu hawa wamesema nini? Na wametoka wapi? Naye Hezekia akamujibu: Wamekuja kutoka inchi ya mbali, kule Babeli.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Pahali pake mulisema: Hapana! Sisi tutakimbia na farasi wenye mbio. Sawa, mutakimbia na farasi wenye mbio, lakini farasi wa waadui zenu wana mbio zaidi.


Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa, imepanua kinywa chake mpaka mwisho. Waheshimiwa pamoja na watu wengine wa Yerusalema wanaingia humo makundi kwa makundi, vilevile na wote wanaushangilia kwa furaha.


Watu hao wakaenda mpaka Yordani na katika njia waliona nguo na vifaa vingine Waaramu walivyoacha walipokuwa wanakimbia. Wakarudi na kumupasha mufalme habari.


Basi, Yakobo akasikia kwamba wana wa Labani walinungunika na kusema: “Yakobo amepeleka kila kitu cha baba yetu; ndivyo alivyopata kuwa tajiri.”


Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.


Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia; inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.


Siku hiyo, utukufu wa Yakobo utaporomoshwa, na unono wake utapotea.


Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaazibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.


Yawe wa majeshi atakuja kukusaidia; atakuja na ngurumo, tetemeko la inchi na sauti kubwa; atakuja na upepo mukali, zoruba na moto wenye kuunguza.


wote watapata haya. Wamisri hawawezi kuwasaidia ninyi, hawawezi kuwapa musaada au faida, lakini watawapatisha haya tu na kuwafezehesha.


Maana musaada wa Misri ni bure, haufai kitu; kwa hiyo nimeipanga Misri jina: Nyoka mukubwa asiyekuwa na nguvu!


Nawe Yerusalema uliyeachwa tupu, kwa nini sasa unavaa nguo nzuri nyekundu? Kwa nini kujipamba kwa zahabu, na kujipakaa wanja kwenye macho? Unajipamba bure! Wapenzi wako wanakuzarau sana; wanatafuta kukuua tu.


Nitalia na kuomboleza juu ya milima; nitaomboleza juu ya mashamba ya nyama katika jangwa, kwa sababu yamekauka kabisa, hakuna mutu anayepita pahali pale. Hakusikiliki tena sauti za ngombe; ndege na nyama wamekimbia na kutoweka.


Nitawatayarisha waangamizaji wakufikie, kila mumoja akishika silaha yake. Watazikata nguzo zako nzuri za mierezi, na kuzitumbukiza katika moto.


Mutafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa, au katika karamu ya Yawe?


Mutu muzuri zaidi kati yao ni kama michongoma, naye mwenye usawa zaidi ni hatari kama upango wa miiba. Siku iliyongojewa ya azabu yao imefika. Na sasa mahangaiko yamewapata.


Kwenu itakuwa kama anayejinyoosha juu ya kitanda kifupi sana, au kujifunika kwa blanketi inayokuwa ndogo sana!


Mambo yatakuwa kama mutu aliyekimbia simba, halafu anakutana na dubu! Au kama mutu anayerudi kwa nyumba yake, na kutia mukono wake kwenye ukuta, na kuumwa na nyoka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite