Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!

Gade chapit la Kopi




Isaya 1:3
24 Referans Kwoze  

Hata korongo anajua wakati wa kuhama; njiwa, mbaruwayi na koikoi, wanajua nyakati zao za kurudi. Lakini hawa watu wangu hawajui maagizo ya Yawe.


Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.


Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefungwa macho wasipate kuona na akili wasipate kufahamu.


Katika karamu zao, hapakosekani vinubi, zeze, ngoma, filimbi na divai. Lakini hawajali matendo ya Yawe, wala kutambua kazi za mikono yake.


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Enyi wajinga wa mwisho, mufikiri kidogo! Enyi wapumbafu, mutapata akili wakati gani?


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Watu hawa wanasahau kwa makusudi kwamba tangia zamani Mungu alisema tu, na mbingu na dunia vikakuwa. Dunia iliumbwa toka katika maji na kwa njia ya maji.


Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu, fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.


Mwanadamu ni mujinga na mupumbafu; kila mufua zahabu anafezeheshwa na sanamu zake. Sanamu hizo ni uongo mutupu, hazina uzima wowote ndani yao.


Wote ni wajinga na wapumbafu, fundisho la sanamu hizi ni mazarau matupu!


Pahali zile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia, ni mufano wa watu wanaosikia habari ya Ufalme na kukosa kuielewa. Na kisha yule mwovu Shetani anakuja na kuondoa mbegu zilizopandwa ndani ya mioyo yao.


Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.


Hao ni kama imbwa walafi sana, wala hawawezi kutosheka hata kidogo. Wachungaji nao hawana akili yoyote. Kila mumoja anatafuta njia yake mwenyewe, kila mumoja anatafuta faida yake.


Kweli wewe ni mugonjwa wa mapenzi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Unafanya uzinzi bila kuona haya hata kidogo.


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


Waovu hawaelewi haki ya sheria, lakini wanaomwogopa Yawe wanaielewa kabisa.


Ninyi mumeona mambo mengi, lakini hamuelewi kitu. Masikio yenu yako wazi, lakini hamusikii kitu!


Wana wa Yonadabu mwana wa Rekabu wameshika amri waliyopewa na babu yao; lakini ninyi hamukunitii.


Watu wangu walikuwa kama kondoo waliopotea; wachungaji wao wamewapotosha, wakawageuza kuelekea kwenye milima; walitembea toka mulima mpaka kilima, wakasahau makao yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite