Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 1:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Mutapata haya kwa ajili ya miti ya mialo muliyoipenda sana; mutafezeheka kwa sababu ya bustani mulizofurahia.

Gade chapit la Kopi




Isaya 1:29
17 Referans Kwoze  

Kuna watu wanaojitakasa na kujisafisha wapate kuingia kwenye bustani za ibada za sanamu; wanafanya maandamano na kuhani akiwa kati yao. Watu wale wanakula nguruwe, panya na vyakula vingine vyenye kuwa machukizo. Watu wale hakika watakufa wote pamoja. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Ni watu ambao wananichokoza waziwazi siku zote; wanatambikia miungu yao katika bustani, na kuifukizia ubani juu ya matofali.


Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.


Wanatambikia kwenye vilele vya milima; wanatoa sadaka kwenye vilima, chini ya miti ya mwalo, migude na mikwaju, maana kivuli chao ni kizuri. Kwa hiyo wabinti wenu wanafanya uzinzi, na bibi-arusi wenu anafanya uasherati.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!


Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Kisha mutakapokumbuka mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya, mutajichukia wenyewe kwa sababu ya maovu yenu na machukizo muliyofanya.


Wakati maiti zao zitakapokuwa zimelala kati ya sanamu zao za miungu, na kwenye mazabahu zao juu ya kila mulima, chini ya kila muti wenye kivuli, chini ya kila muti wa mwalo wenye majani na popote walipotolea sadaka zenye harufu nzuri ya kuzipendeza sanamu zao za miungu. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Katika siku ya utawala wa mufalme Yosia, Yawe aliniambia hivi: Umeona jinsi yule Israeli asiyekuwa mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila muti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake kule!


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Watengenezaji wa sanamu watapata haya na kuzarauliwa, wote pamoja watafezeheka.


Wakati utafika ambapo ninyi wote mutatupilia mbali sanamu zenu za feza na zahabu ambazo mumejitengenezea kwa mikono yenu inayowakosesha.


Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!


Wote wanaotegemea sanamu za miungu, wote wanaoziambia “Ninyi ni miungu yetu” watakomeshwa na kupata haya.


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite