Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 1:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!

Gade chapit la Kopi




Isaya 1:2
37 Referans Kwoze  

Utege sikio, ee mbingu. Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.


Ninaita mbingu na inchi zishuhudie juu yenu leo hii, kwamba nimewapa uchaguzi kati ya uzima na kifo, kati ya baraka na laana. Basi, muchague uzima ninyi na wazao wenu mupate kuishi.


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Kutoka juu anaita mbingu na dunia kuwa washuhuda wake atakapowahukumu watu wake.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoto anamuheshimu muzazi wake, na mutumishi anamuheshimu bwana wake. Ikiwa mimi ndiye Baba wenu, mbona munanivunjia heshima? Ikiwa mimi ni bwana wenu, mbona hamuniheshimu? Ninasema hivyo kwa ninyi makuhani munaozarau jina langu. Nanyi munauliza: Sisi tumezarau jina lako namna gani?


Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Kwa hiyo, enyi milima ya Waisraeli, musikie neno la Bwana wenu Yawe. Anasema juu ya ninyi milima na vilima, mifereji na mabonde, jangwa tupu na miji ya matongo, na miji iliyokamatwa mateka na kuzarauliwa na mataifa yote yanayowazunguka.


Ee inchi, ee inchi, ee inchi! Sikia neno la Yawe!


Sikiliza, ee dunia! Mimi nitawaletea watu hawa hasara kulingana na nia zao mbaya. Maana hawakuyajali maneno yangu, na mafundisho yangu nayo wameyakataa.


Muchana kutwa niliwanyooshea mikono watu waasi, watu ambao wanafuata njia zisizokuwa nzuri, watu ambao wanafuata mawazo yao wenyewe.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Watarudi wakiwa wanatoa machozi, nami nitawaongoza nikiwafariji; nitawapitisha kando ya vijito vya maji, katika njia iliyonyooka ambamo hawatajikwaa; maana mimi nimekuwa baba wa Israeli, Efuraimu ni muzaliwa wangu wa kwanza.


Enyi Waisraeli, musikilize kwa uangalifu, musikuwe na kiburi maana Yawe anasema nanyi.


kule katika jangwa ambako muliona jinsi alivyowabeba safari hiyo yote kama vile baba anavyobeba mwana wake, mpaka mukafika hapa.


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora.


Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.


Mujongee musikilize enyi mataifa, musikilize enyi watu. Sikiliza, ee dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, ulimwengu na vyote vinavyotoka humo!


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu. Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.


Uwape mufano hao watu wangu waasi na kuwaambia kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Weka chungu juu ya mafika, ukijaze maji vilevile.


Alimwacha Yawe, Mungu wa babu zake. Hakushika njia ya Yawe.


Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite