Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Isaya 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Musikilize neno la Yawe, enyi watawala waovu kama wa Sodoma! Musikilize mafundisho ya Mungu wetu, enyi watu waovu kama wa Gomora!

Gade chapit la Kopi




Isaya 1:10
21 Referans Kwoze  

Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Kwangu mimi, ninyi Waisraeli, muko sawasawa na watu wa Kushi! –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwatoa Wafilistini kutoka Krete, na Waaramu kutoka Kiri, kama nilivyowatoa ninyi kutoka Misri.


Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Maana mizabibu yao ni mizabibu ya Sodoma, zimetoka katika mashamba ya Gomora. Zabibu zake ni zabibu zenye sumu, vishada vyake ni vichungu.


Ni kama vile Isaya alivyokuwa ametangulia kusema: “Kama Bwana wa Majeshi hangetuponyeshea wamoja wa wazao wetu, ingetutokea sawa Sodoma, ingegeuka kwetu sawa Gomora.”


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Basi, musikilize neno la Yawe, enyi wenye mazarau munaotawala watu wa Yerusalema:


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Wewe mwanadamu, uwakaripie manabii wa Waisraeli wanaotangaza mambo ambayo wameyafikiria wao wenyewe. Uwaambie: Musikilize neno la Yawe!


Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.


Sasa basi, ewe kahaba, usikilize neno la Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite