Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 9:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.

Gade chapit la Kopi




Hosea 9:9
16 Referans Kwoze  

Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


Walipokuwa kule muzee mumoja akafika kutoka kwa shamba lake. Muzee huyo alikuwa mutu wa inchi ya milima ya Efuraimu na alikuwa akiishi kule Gibea kama mugeni. Wakaaji wa muji wa Gibea walikuwa wa kabila la Benjamina.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Bwana wake akamujibu: “Hatutageuka na kuingia katika muji wa wageni ambao si Waisraeli. Tutaendelea na safari mpaka Gibea.


Waisraeli waliwazunguka watu wa kabila la Benjamina, wakawafuatilia kutoka Noha mpaka upande wa mashariki wa muji wa Gibea wakiwaua wengi kati yao.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani; nitawaazibu kwa sababu ya mwenendo wao, nitawalipiza matendo yao wenyewe.


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Hawafikiri hata kidogo kwamba mimi ninayakumbuka maovu yao yote. Sasa maovu yao yamewabana. Yote waliyotenda yako mbele yangu.


Nabii ni mulinzi wa Waefuraimu kwa pahali pa Mungu; lakini, popote anapoenda anategewa mutego kama ndege. Hata katika nyumba ya Mungu wake anachukiwa.


Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii na kukubali kuonywa; hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu. Lakini watu wake walizidisha tamaa zao za kufanya matendo yao kuwa upotovu.


Yawe akamwambia Musa: Teremuka chini kwa maana watu wako uliowaleta kutoka inchi ya Misri wamejipotosha wenyewe.


Walipokuwa wanajifurahisha, kumbe wanaume watenda maovu wa muji ule wakakuja wakaizunguka nyumba ile na kugonga kwa mulango. Wakamwambia muzee mwenye nyumba: “Umutoshe inje yule mwanaume aliyekuja kwako, tulale naye.”


Lakini watu wa Yerusalema watauzania kuwa ni utabiri wa uongo kwa sababu ya mapatano waliyofanya. Hata hivyo unabii huu utawakumbusha uovu wao na kusababisha kukamatwa kwao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite