Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 9:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Watu wa Efuraimu wamepigwa, wamekuwa kama muti wenye muzizi wenye kukauka, hawatazaa watoto wowote. Hata kama wakizaa watoto, nitawaua watoto wao wanaowapenda.

Gade chapit la Kopi




Hosea 9:16
10 Referans Kwoze  

Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota, hata mbele hawajatoa mizizi kama miti katika udongo, Yawe akiwapulizia wananyauka, upepo mukali unawapeperusha kama makapi!


Yeye ni kama muti uliokauka mizizi, matawi yake juu yamenyauka.


Halafu yakafuatwa na masuke mengine saba matupu, membamba na yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa.


Vita itasababisha vifo vingi inje, na ndani ya nyumba hofu itawatawala. Vijana wanaume na wanawake watauawa, hata wenye kunyonya na wazee wenye imvi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite