Watu wa Efuraimu wamepigwa, wamekuwa kama muti wenye muzizi wenye kukauka, hawatazaa watoto wowote. Hata kama wakizaa watoto, nitawaua watoto wao wanaowapenda.
Hapo hasira yangu itawawakia siku hiyo, nami nitawaacha na kuficha uso wangu mbali nao, wataangamizwa. Maovu mengi na taabu zitawapata hata watambue kwamba maovu hayo yamewapata kwa sababu Mungu wao hayuko kati yao.
Zamani, niliona kwamba Efuraimu ilikuwa kama muti wa ngazi muchanga kwenye nafasi nzuri. Lakini sasa Efuraimu italazimishwa kuwapeleka watoto wake wauawe.
Nimepepeta watu wangu kwa kuwasambaza sawa maganda, toka katika kila muji wa inchi yao. Nimewaangamiza kwa kuwaua watoto wao, lakini hawakuacha mwenendo wao.
mpaka kwa mwisho Yawe akawafukuza kutoka mbele yake, kama vile alivyokuwa amesema kupitia kwa watumishi wake wote manabii. Kwa hiyo watu wa Israeli walipelekwa katika uhamisho kutoka katika inchi yao wenyewe mpaka Asuria ambako wanakaa hata sasa.
Watoto wenu wanaume na wanawake watatolewa kwa watu wengine nanyi mutakodoa macho muchana kutwa kuwatazamia warudi, lakini hamutakuwa na nguvu ya kufanya chochote.
Yawe alikuwa amesema kwamba wote watakufia katika jangwa, na kweli hakuna hata mumoja wao aliyebaki muzima, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, na Yoshua mwana wa Nuni.
Yawe awatenge mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka kati ya wazao wa Yakobo. Na wasishiriki hata kidogo katika kutoa ushuhuda na kuleta sadaka mbele ya Yawe wa majeshi.
Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.
Umewaalika kama kwenye sikukuu waadui zangu walionitisha kila upande. Katika siku ya hasira yako, ee Yawe, hakuna aliyetoroka au kubakia. Wale niliowazaa na kuwalea, waadui zangu wamewaangamiza.