Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

Gade chapit la Kopi




Hosea 8:4
20 Referans Kwoze  

Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Mimi ni muchungaji mwema. Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua,


Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


Lakini atawaambia tena: ‘Sijui munatokea wapi. Mutoke karibu nami, ninyi wote watenda maovu!’


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Lakini bwana akajibu: ‘Kweli ninawaambia: mimi siwajui ninyi.’ ”


Mutupilie mbali zambi mulizonitendea; mujipatie moyo na roho mupya. Enyi Waisraeli, mutakufa kwa sababu gani?


Tendo hili likakuwa zambi ambayo ilisababisha ukoo wa Yeroboamu ufutiliwe mbali na kuangamizwa.


Mwanadamu anaweza kujitengenezea miungu? Kweli hiyo si miungu hata kidogo!


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Lakini Waisraeli wametupilia mambo mazuri. Kwa hiyo, sasa waadui watawafuatilia.


Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka; Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli, lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.


Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme, kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite