Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.

Gade chapit la Kopi




Hosea 8:14
31 Referans Kwoze  

Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Basi, nitashusha moto juu ya inchi ya Yuda, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Yerusalema.


Lakini mulipokwisha kula na kushiba, mulianza kuwa na kiburi, mpaka mukanisahau.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Tiro, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri.


Kwa maana sisi ni viumbe vya Mungu, na kwa kuungana kwetu na Yesu Kristo, alituumba kusudi tuishi maisha ya matendo mema, ambayo Mungu alitutayarishia tangu mbele tupate kuyatenda.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.


Basi, nitashusha moto juu ya muji wa Temani, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za Bosira.


Basi, nitashusha moto juu ya nyumba ya mufalme Hazaeli, na kuziteketeza kabisa nyumba nzuri za mufalme Beni-Hadadi.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Kwa ndoto hizo zao wanafikiri kwamba watawashawishi watu wangu wanisahau mimi kama vile babu zao walivyonisahau, na kumufuata mungu Bali!


Kelele linasikilika juu ya vilima: Waisraeli wanalia na kuomboleza, kwa sababu wamepotoka katika njia zao, wamenisahau mimi Yawe, Mungu wao.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe, kusudi wazitangaze sifa zangu!


Kwa hiyo aliwamwangia kasirani yake kali, akawaacha kupatwa na vita kali. Hasira yake iliwawakia kila upande, lakini wao hawakuelewa chochote; iliwachoma, lakini hawakufikiri juu ya jambo hilo.


Yawe anajitokeza kama shujaa; kama vile askari katika vita anatatanua kupigana. Anapiga kelele kubwa la vita na kujionyesha mwenye nguvu juu ya waadui zake.


Watakapowaona watoto wao, watoto niliowajalia mimi mwenyewe, watalitukuza jina langu mimi Mutakatifu wa Yakobo, watakuwa na heshima kwangu mimi Mungu wa Israeli.


Walimusahau Mungu aliyewaokoa, aliyetenda mambo makubwa katika inchi ya Misri,


Alijenga miji kwenye inchi ya milima ya Yuda, na kwenye pori, akajenga makimbilio na minara katika milima yenye pori.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Vilevile, Yeroboamu alijenga nafasi ya kutambikia juu ya vilima, akachagua makuhani ambao hawakukuwa wa ukoo wa Lawi.


Katika mwaka wa kumi na ine wa utawala wa mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria aliishambulia miji yote yenye kuta ya Yuda na kuiteka.


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


Kuta za matofali zimeanguka lakini sisi tutazijenga kwa mawe yaliyochongwa! Nyumba za nguzo za mikuyu zimeharibiwa lakini pahali pake tutajenga za mierezi.


Basi, Yawe atawaletea wapinzani na kuwachochea waadui zao.


Watakula mazao yenu na chakula chenu; watawaua wana na wabinti zenu. Watachinja makundi yenu ya kondoo na ngombe; wataiharibu mizabibu yenu na miti yenu ya matunda ya tini. Miji yenu yenye kuzungukwa na kuta munayoitegemea, wataiharibu kwa silaha zao.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa kuwa umenisahau na kunigeuzia mugongo, basi, utabeba muzigo wa uasherati na uzinzi wako.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite