Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Gileadi ni muji wa waovu, umejaa damu.

Gade chapit la Kopi




Hosea 6:8
17 Referans Kwoze  

Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.


Wakamusihi Festo awafanyie wema kwa kuwaletea Paulo Yerusalema, kwa maana walikuwa wakivizia kumwua katika njia.


Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.


Wavu wenu haufai kama nguo, watu hawawezi kujifunikia munachofuma. Kazi zenu ni kazi za uovu, matendo yenu yote ni mateso makali.


Ee Mungu wangu, uniokoe kutoka waadui zangu, unikinge na hao wanaonishambulia.


Anajificha karibu na vijiji akivizia, amwue kwa siri mutu asiyekuwa na kosa. Yuko macho kumuvizia muzaifu;


“Zaidi ya hayo, unajua vilevile yale Yoabu mwana wa Zeruya aliyonitendea, jinsi alivyowatendea majemadari wawili wa waaskari wa Israeli, Abeneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yeteri. Aliwaua wakati wa amani akitaka kulipiza kisasi kwa mauaji waliyofanya wakati wa vita. Aliwaua watu wasiokuwa na kosa, nami nikabeba lazima ya kifo cha watu wale kwa ajili ya vitendo vyake.


Walipofika kwenye jiwe kubwa linalokuwa kule Gibeoni, Amasa akatoka kwenda kuwapokea. Yoabu alikuwa akivaa nguo ya kiaskari, na ndani ya nguo ile kulikuwa mukaba ulioshikilia upanga kwenye kiuno chake ukiwa kwenye mufuko wake. Yoabu alipokuwa anakaribia, upanga wake ulichomoka ndani ya mufuko ukaanguka chini.


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Katika eneo la kabila la Gadi walipewa Ramoti wa Gileadi, muji wa kukimbilia usalama, pamoja na mbuga zake za malisho, Mahanaimu pamoja na mbuga zake za malisho,


Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.


Watu wa Gileadi walikuwa waovu sana; hakuna tena kitu kinachokuwa chao. Kule Gilgali walitambikia ngombe dume. Hivyo, mazabahu zao zitakuwa malundo ya mawe yaliyowekwa kwa mafungu katika shamba.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite