Hosea 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 20028 Gileadi ni muji wa waovu, umejaa damu. Gade chapit la |
“Zaidi ya hayo, unajua vilevile yale Yoabu mwana wa Zeruya aliyonitendea, jinsi alivyowatendea majemadari wawili wa waaskari wa Israeli, Abeneri mwana wa Neri, na Amasa mwana wa Yeteri. Aliwaua wakati wa amani akitaka kulipiza kisasi kwa mauaji waliyofanya wakati wa vita. Aliwaua watu wasiokuwa na kosa, nami nikabeba lazima ya kifo cha watu wale kwa ajili ya vitendo vyake.
Walipofika kwenye jiwe kubwa linalokuwa kule Gibeoni, Amasa akatoka kwenda kuwapokea. Yoabu alikuwa akivaa nguo ya kiaskari, na ndani ya nguo ile kulikuwa mukaba ulioshikilia upanga kwenye kiuno chake ukiwa kwenye mufuko wake. Yoabu alipokuwa anakaribia, upanga wake ulichomoka ndani ya mufuko ukaanguka chini.