Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mumechimba shimo refu la kuwanasa kule Sitimu. Lakini mimi nitawaazibu ninyi wote.

Gade chapit la Kopi




Hosea 5:2
18 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.


Ole kwenu ninyi munaomuficha Yawe mipango yenu, munaotenda matendo yenu katika giza na kusema: Hakuna atakayetuona; nani anayeweza kujua tunachofanya?


Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.


Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.


Ndiyo maana ninawashambulia kwa njia ya manabii, nimewaangamiza kwa maneno yangu, hukumu yangu inajitokeza kama mapambazuko.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Wote ni waasi na wagumu, ni watu wanaopitapita wakisengenya wengine, ni wagumu kama shaba au chuma. Wote wanatenda mabaya.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite