Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.

Gade chapit la Kopi




Hosea 4:6
54 Referans Kwoze  

Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.


Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


‘Watu hawa wananiheshimu kwa midomo yao. Lakini mioyo yao ni mbali nami.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Nao makuhani hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe? Wafundi wa sheria hawakunijua, viongozi wa watu waliniasi; manabii nao walitabiri kwa jina la Bali na kuabudu sanamu zisizokuwa na faida yoyote.


Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.


Lakini mulipokwisha kula na kushiba, mulianza kuwa na kiburi, mpaka mukanisahau.


Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Yawe anasema: Watu wangu ni wapumbafu, hawanijui mimi. Wao ni watoto wajinga; hawana ufahamu. Wao wanaelewa vizuri kutenda maovu, lakini hawajui kutenda mema.


Lakini wasipomutii, wanaangamia kwa upanga, na kufa kwa kukosa akili.


Musikilize, enyi wajinga na wapumbafu: ninyi munaokuwa na macho, lakini hamwoni, munaokuwa na masikio, lakini hamusikii.


Watu wangu watateswa na watoto; wanawake ndio watakaowatawala. Enyi watu wangu, wakubwa wenu wanawapotosha, wanavuruga njia munayopaswa kufuata.


Upendo wangu kwako unanifanya niwake hasira, maana waadui zangu hawajali maneno yako.


Waovu wametega mitego waninase, lakini mimi sisahau sheria yako.


Muwaache! Wao ni vipofu, wanaongoza vipofu wengine. Na kama kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili wanatumbukia ndani ya shimo.”


Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi, wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.


Mupige baragumu! Adui anakuja kama tai kuishambulia nyumba ya Yawe, kwa sababu wamelivunja agano langu na kuiasi sheria yangu.


Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Wana wa Eli walikuwa wapotovu sana. Hawakumujali Yawe


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Uangalie mateso yangu, uniokoe, kwa maana sikusahau sheria yako.


Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.


Makuhani watafundisha taifa langu kupambanua vitu vinavyokuwa vitakatifu na visivyokuwa vitakatifu, na kuwajulisha tofauti kati ya vitu vinavyokuwa vichafu na visivyokuwa vichafu.


Lakini sitawaazibu wabinti zenu wanapofanya uzinzi, wala bibi-arusi wenu wanapofanya uasherati, maana, wanaume wenyewe ndio wanaofuatana na wazinzi, na kutambikia pamoja nao katika ibada za uzinzi. Watu hawa wenye kukosa akili hakika wataangamia!


Matendo yao yanawazuia wasimurudilie Mungu wao. Wamejaa uzinzi ndani ya mioyo yao; hawanijui mimi Yawe.


Wageni wamenyonya nguvu zake, wala yeye mwenyewe hajui; imvi zimejaa juu ya kichwa chake, lakini yeye mwenyewe hana habari.


Efuraimu ni kama njiwa mujinga asiyekuwa na akili; mara yuko Misri, mara Asuria kwa kuomba musaada.


bila kosa kwa wale ambao hawafanyi makosa, lakini mukali kwa waovu.


Na ukimupa mutu yeyote asiyejua kusoma, na kumwambia “Unisomee kitabu hiki”, atasema: “Sijui kusoma.”


Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite