Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.

Gade chapit la Kopi




Hosea 2:8
27 Referans Kwoze  

Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.


Uasherati, divai mupya na ya zamani vinaondoa maarifa.


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.


Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao, na kuzifukizia ubani; maana kwa njia ya vitu hivyo mapato yao yanaongezeka, na wanakuwa na chakula kingi.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Pahali pake umejitukuza mwenyewe mbele ya Bwana wa mbinguni: umeleta vyombo vya nyumba ya Mungu ukavitumia kwa kunywea divai, wewe, wakubwa wako, wanawake wako na wahabara wako, na kuisifu miungu iliyotengenezwa na feza, zahabu, shaba, chuma, miti na mawe; miungu ambayo haioni, haisikii wala haijui jambo lolote. Lakini Mungu, ambaye uzima wako uko katika mukono wake, na njia zako ziko wazi mbele yake, haukumuheshimu!


Watoto wanaokota kuni, wababa wanawakisha moto na wamama wanaponda unga kwa ajili ya kutengeneza mikate ya kumutambikia mungu wa kike, wanayemwita malkia wa mbinguni. Tena wananikasirikisha kwa kuitolea miungu mingine sadaka ya divai.


Watu wanapoteza zahabu kutoka mifuko yao, wanapima feza kwenye mizani zao, wanamulipa mufuaji wa zahabu awatengenezee sanamu ya mungu, kisha wanainama mbele yake na kuiabudu!


Wakatoka na kwenda kwenye mashamba yao ya mizabibu, wakachuma zabibu halafu wakazikamua, wakatengeneza divai wakafanya sikukuu. Wakaingia kwenye nyumba ya mungu wao wakakula na kunywa, kisha wakamutukana Abimeleki.


Waisraeli walikuwa kama muzabibu muzuri, muzabibu wenye kuzaa matunda. Kadiri matunda yalivyozidi kuongezeka, ndivyo walivyozidi kujijengea mazabahu. Kadiri inchi yao ilivyozidi kustawi, ndivyo walivyozidi kupamba nguzo zao za ibada.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye anayewapa uwezo wa kupata utajiri. Anafanya hivyo kwa kuimarisha agano alilofanya na babu zenu mpaka leo.


Kisha wakaikaa kwenye vitanda vizurivizuri, na mbele yao meza imetandikwa. Juu ya meza hiyo uliweka ubani wangu na mafuta yangu.


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka; Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli, lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.


Ee Yawe, Mungu wetu, wingi wote huu tuliotoa kwa kukujenga nyumba kwa ajili ya utukufu wa jina lako takatifu, unatoka katika mukono wako na yote ni yako.


Njia yangu ameiziba kwa ukuta kusudi nisipite, njia zangu amezitia giza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite