Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 2:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali, kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani, akajipamba kwa pete zake na ushanga, na kuwaendea wapenzi wake, akanisahau mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.

Gade chapit la Kopi




Hosea 2:15
33 Referans Kwoze  

Watakaa humo kwa salama kabisa; watajenga nyumba na kupanda mizabibu. Wataishi bila hofu maana mataifa jirani zao ambayo yaliwauzi, mimi nitayaazibu. Hapo watatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao.


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


Halafu wakalundika mawe mengi juu yake, ambayo yako mpaka leo. Hapo hasira ya Yawe ikapoa; na pahali pale pakaitwa Bonde la Akori, ni kusema Bonde la Taabu, mpaka hivi leo.


Walipofika Antiokia, wakafanya mukutano wa kanisa na kuwaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao, na namna alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mulango kusudi wao vilevile wapate kuamini.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Nitarudisha hali ya mbele ya watu wangu Waisraeli. Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi ndani yake; watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima mashamba na kula mazao yake.


Lakini mimi nitalikumbuka agano langu nililoagana nawe katika siku za ujana wako. Nitafanya nawe agano la milele.


Katika machukizo yako yote pamoja na uzinzi wako haukuzikumbuka siku za utoto wako, wakati ulipokuwa uchi kabisa, bila kitu, ukigaagaa katika damu yako!


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Watu watajenga nyumba na kuishi humo; watalima mizabibu na kula matunda yake.


Enyi wafungwa wenye tumaini, murudi kwenye ukuta wa muji wenu. Sasa mimi ninawatangazia: nitawarudishia mema mara mbili.


Lakini ninakumbuka jambo hili moja, nami ninakuwa na tumaini:


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nyumba na mashamba, pamoja na mashamba ya mizabibu katika inchi hii yatanunuliwa tena.


Hapo watu wake wakaamini maneno yake, wakamwimbia nyimbo za sifa yake.


Hapo Waisraeli wakaimba wimbo huu: Bubujika maji, ee kisima! Muimbe!


Efuraimu amesema: Mimi ni tajiri! Mimi nimejitajirisha! Sikufanya mabaya kwa kupata hii faida.


Bonde la Saroni litakuwa nafasi ya kukulishia nyama, bonde la Akori litakuwa mapumziko ya ngombe kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.


Nitamuvua nguo abaki uchi mbele ya wapenzi wake, wala hakuna mutu atakayeweza kunizuia.


Wimbo wa safari za kidini. Kila mutu katika Israeli aseme: “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu”.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Na sasa hivi tu unanililia, ukisema: Wewe ni baba yangu, ulinipenda tangu utoto wangu?


Maana, mimi ninajua mupango ninaokuwa nao juu yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nayo mipango yangu ni ya kuwatendea mema wala si mabaya, kusudi mupate kuwa na tumaini katika siku zinazokuja.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walisambazwa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kwamba mimi ni mutakatifu. Waisraeli wataishi katika inchi yao ambayo mimi nilimupa mutumishi wangu Yakobo.


Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Waisraeli wakamusahau Yawe, Mungu wao, aliyewakomboa kutoka kwa waadui zao wengi waliowazunguka kila upande.


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite