Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 2:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.

Gade chapit la Kopi




Hosea 2:13
44 Referans Kwoze  

Lakini mulipokwisha kula na kushiba, mulianza kuwa na kiburi, mpaka mukanisahau.


Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe. Wakamusahau Yawe, Mungu wao, wakaabudu Mabali na Maashera.


Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka; Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli, lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Munaiba, munaua, munafanya uzinzi, munaapa kwa uongo, munamufukizia mungu Bali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamujapata kuijua.


Siku za azabu zimetimia, siku za kulipiza kisasi zimefika; Waisraeli lazima wautambue wakati huo! Ninyi munasema: Nabii ni mupumbafu; anayeongozwa na roho ni mwenda-wazimu. Munasema hivyo kwa sababu ya uovu wenu mukubwa, kwa sababu ya chuki yenu kali juu yake.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Wanatambikia kwenye vilele vya milima; wanatoa sadaka kwenye vilima, chini ya miti ya mwalo, migude na mikwaju, maana kivuli chao ni kizuri. Kwa hiyo wabinti wenu wanafanya uzinzi, na bibi-arusi wenu anafanya uasherati.


Mama yao amefanya uzinzi, aliyebeba mimba yao amefanya mambo ya haya. Alisema: Nitaambatana na wapenzi wangu, ambao wananipatia chakula na maji, nguo za sufu na kitani, pamoja na mafuta na divai.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa kuwa umenisahau na kunigeuzia mugongo, basi, utabeba muzigo wa uasherati na uzinzi wako.


Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Ulitwaa vile vitu vyako vizuri vya zahabu na feza nilivyokupa kwa kujipamba, ukajifanyia sanamu za wanaume upate kufanya uzinzi nazo.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: Ninyi munasambaza kondoo wangu na kuwafukuza, wala hamukuwatunza. Basi, nami vilevile nitawaazibu kwa ajili ya matendo yenu maovu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini watu wangu wamenisahau mimi, wanaifukizia miungu ya uongo ubani. Wamejikwaa katika njia zao, wameacha barabara zao za zamani.


Enyi watu wa Yuda, hesabu ya miji yenu ni sawasawa na hesabu ya miungu yenu. Na kama vile barabara zenu za Yerusalema zinavyokuwa nyingi, ndivyo mulivyojenga mazabahu ya haya, ni kusema ya kufukizia ubani kwa mungu Bali.


Kijana binti anaweza kusahau mapambo yake, au bibi arusi nguo yake? Lakini watu wangu wamenisahau kwa muda wa siku zisizohesabika.


Maana wewe Israeli umemusahau Mungu aliyekuokoa, haukukumbuka Jiwe lako la kufichamia. Kwa hiyo, hata mukipanda mimea ya Bali, na kuitakasa kwa mungu wa kigeni;


Walimusahau Mungu aliyewaokoa, aliyetenda mambo makubwa katika inchi ya Misri,


Lakini bila kukawia walisahau matendo yake, wakaacha kutegemea shauri lake.


Walisahau mambo aliyokuwa ametenda, ndiyo miujiza aliyokuwa amewaonyesha.


Ndivyo wote wanaomusahau Mungu wanavyokuwa. Tumaini la wasiomwamini Mungu litapotea.


Alitengeneza upya nafasi za kuabudia miungu mingine zilizoharibiwa na baba yake Hezekia. Akajenga mazabahu za kuabudia Bali na kutengeneza sanamu ya Ashera, kama vile Ahabu mufalme wa Israeli alivyofanya. Vilevile, Manase aliabudu na kutumikia jeshi la mbingu.


Hivi ndivyo Yehu alivyomaliza ibada za Bali katika Israeli.


Mufalme Ahazia alipokuwa Samaria alianguka kutoka chumba kilichokuwa juu ya paa ya nyumba yake, akaumia vibaya. Kwa hiyo akawatuma wajumbe, akawaambia: “Muende kwa Bali-Zebubu, mungu wa muji wa Ekuroni, mumwulize kama nitapona ugonjwa huu.”


Lakini wao walimusahau Yawe, Mungu wao, naye akawatia katika mikono ya Sisera, jemadari wa waaskari wa muji wa Hazori, na katika mikono ya Wafilistini na katika mikono ya mufalme wa Moabu. Mataifa hayo yalipigana na babu zenu na kuwashinda.


Waisraeli wakatenda tena uovu mbele ya Yawe, wakatumikia Mabali, Mastaroti, na miungu ya Aramu, ya Sidona, ya Moabu, ya Amoni na ya Wafilistini. Wakamwacha Yawe wala hawakumwabudu tena.


Hamukumujali Mulima wenu, yule aliyewapa uzima. Mulimusahau Mungu aliyewazaa ninyi.


muhakikishe kwamba hamutamusahau Yawe aliyewatoa Misri ambako mulikuwa watumwa.


Lakini sasa kwenda uwaongoze watu mpaka pahali nilipokuambia. Malaika wangu atakutangulia. Hata hivyo, siku nitakapowafikia, nitawaazibu kwa sababu ya zambi yao.


Nitawalipiza maovu yao wayalipe vilevile maovu ya babu zao. –Ni Yawe anayesema hivyo.– Wao waliifukizia ubani miungu yao kwenye milima, wakanitukana mimi kule juu ya vilima. Nitawalipa sawa inavyostahili, watayalipa matendo yao ya zamani.


Nikakutia pete kwenye pua, visikio kwenye masikio yako na juu ya kichwa chako nikakupamba kwa taji nzuri.


Inchi itakuwa jangwa na katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalema nitakomesha sauti zote za furaha na shangwe, nazo nyimbo za wenye kufanya ndoa, kwa sababu inchi itakuwa ukiwa.


Barabara za Sayuni zinaomboleza, maana hakuna anayepita kwa sikukuu. Milango yake yote ni tupu, makuhani wake wanaugua, wabinti zake wana huzuni, na muji wenyewe uko katika uchungu.


Wazee wameacha kutoa mashauri yao, vijana wameacha kuimba.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite