Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 14:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.

Gade chapit la Kopi




Hosea 14:4
30 Referans Kwoze  

Niliona mwenendo wao, lakini nitawaponyesha; nitawaongoza na kuwapa faraja, nitawatuliza hao wanaoomboleza.


Siku hiyo mutasema: Ninakushukuru, ee Yawe, maana ingawa ulinikasirikia, hasira yako imetoweka, nawe umenifariji.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu. Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Lakini wakati Mungu Mwokozi wetu alipoonyesha wema wake na upendo wake kwa watu,


Yeye ndiye aliyetuokoa na kutuita kuwa watu wake, si kwa sababu ya matendo lakini ni kwa sababu ya mupango wake mwenyewe na neema yake aliyotupatia katika kuungana na Kristo Yesu mbele ya nyakati zote.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Lakini kwa neema ya Mungu wanahesabiwa haki kwa bure kwa njia ya Kristo Yesu anayewakomboa.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.


Uniponyeshe, ee Yawe, nami nitapona; uniokoe, nami nitaokoka; maana, wewe ndiwe sifa yangu.


Hakuna dawa ya kupakaa kule Gileadi? Hakuna muganga kule? Mbona basi watu wangu hawajaponyeshwa?


Kwa hiyo simba kutoka pori atawaua; imbwa wa pori kutoka jangwa atawararua. Chui anaivizia miji yao. Kila mutu anayetoka humo atararuliwa vipandevipande, kwa sababu zambi zao ni nyingi, maasi yao ni makubwa.


Lakini Mungu mwenye huruma alisamehe uovu wao, wala hakuwaangamiza. Mara nyingi alizuia hasira yake, wala hakuacha kasirani yake yote iwake.


Finehasi mwana wa Eleazari, mujukuu wa kuhani Haruni, ameizuia hasira yangu juu ya Waisraeli; kati yenu ni yeye tu aliyeona wivu kama ule ninaokuwa nao mimi. Ndiyo maana sikuwaangamiza Waisraeli wote kwa hasira yangu.


Basi, Yawe akamwambia Musa: Utwae viongozi wote wa Israeli, uwatundike mbele yangu jua kati, kusudi kasirani yangu juu yenu ipite.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Ee ninyi wote wenye kiu mukuje kwenye maji! Mukuje, wote hata musiokuwa na feza; mununue chakula na mupate kula, mununue divai na maziwa. Bila feza, bila malipo!


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Tena, nikimwambia mutu mwovu kwamba hakika atakufa naye akiacha zambi yake, akianza kutenda mambo yanayokuwa ya haki na sawa, hatakufa.


Hapo mataifa yaliyobaki kandokando yenu, yatatambua kwamba ni mimi Yawe niliyejenga upya yaliyoharibiwa na kupanda mbegu katika inchi iliyokuwa jangwa. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo, na nitafanya hayo.


Lakini wewe unawaona wenye taabu na shida; nawe uko tayari kuwasaidia siku zote. Muzaifu anakutegemea wewe, ee Mungu, wewe umekuwa siku zote musaada wa yatima.


Wamoja wanajivunia magari ya vita, wengine farasi wao. Lakini sisi tunajivunia Yawe, Mungu wetu.


Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite