Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 13:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Basi, nitakuwa kama simba kwenu ninyi wote; nitawavizia kama chui katika njia.

Gade chapit la Kopi




Hosea 13:7
10 Referans Kwoze  

Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efuraimu, kama simba mukali kwa watu wa Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka, nitawakamata na hakuna atakayewaokoa.


Kwa hiyo simba kutoka pori atawaua; imbwa wa pori kutoka jangwa atawararua. Chui anaivizia miji yao. Kila mutu anayetoka humo atararuliwa vipandevipande, kwa sababu zambi zao ni nyingi, maasi yao ni makubwa.


Alikuwa kwangu kama dubu anayevizia, kama simba katika maficho.


Simba akinguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana wetu Yawe akisema, ni nani atakataa kuutangaza ujumbe wake?


Simba ananguruma katika pori kama hajapata nyama? Simba mukali ananguruma katika pango lake kama hajakamata kitu?


Amosi alisema hivi: Yawe ananguruma toka mulima Sayuni, anavumisha sauti yake toka Yerusalema, hata mashamba ya malisho ya wachungaji yanakauka, majani ya mulima Karmeli yananyauka.


Yawe anajitokeza kama shujaa; kama vile askari katika vita anatatanua kupigana. Anapiga kelele kubwa la vita na kujionyesha mwenye nguvu juu ya waadui zake.


Yule nyama niliyemwona alifanana na chui. Miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kinywa chake kilikuwa kama kinywa cha simba. Yule nyoka mukubwa akamupa uwezo wake pamoja na kiti chake cha kifalme na mamlaka makubwa.


Nikiinua kichwa tu, unaniwinda kama simba na kuniponda tena kwa maajabu yako.


Yawe amewaacha watu wake, kama vile simba anavyoacha pango lake; inchi yao imekuwa jangwa tupu, kwa sababu ya vita na hasira kali ya Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite