Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Ni mimi niliyewachunga mulipokuwa katika jangwa, katika inchi iliyokuwa yenye kukauka.

Gade chapit la Kopi




Hosea 13:5
16 Referans Kwoze  

Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.


Ni yeye aliyewaongoza katika lile jangwa kubwa na la kutisha, lenye nyoka wenye sumu na nge katika inchi ile yenye kukauka isiyokuwa na maji, aliwatolea maji kutoka kwenye jiwe gumu.


“Basi, mukumbuke jinsi Yawe Mungu wenu alivyowabariki ninyi katika kila jambo mulilofanya. Aliwatunza mulipokuwa munatangatanga katika jangwa hili kubwa. Amekuwa pamoja nanyi miaka hii yote makumi ine na hamukupungukiwa na kitu chochote.


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


Yawe ni muzuri, yeye ni kimbilio la usalama wakati wa taabu. Yeye anawalinda wote wanaokimbilia usalama kwake.


Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu.


Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea.


Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.


Lakini yule anayemupenda Mungu, huyu anajulikana naye.


Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Ninawachukia wanaoabudu vitu vya bure. Mimi, ninakutumainia wewe, ee Yawe.


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Hivyo, muchana nilivumilia jua kali na usiku baridi ilinipiga. Sikuweza kupata usingizi hata kidogo.


Ninawajua watu wa Efuraimu, Waisraeli hawakufichwa kwangu. Ninyi watu wa Efuraimu mumefanya uzinzi, watu wote wa Israeli wamejichafua.


Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite