Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 13:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia. Lakini yeye ni mutoto mupumbafu; wakati wa kuzaliwa unapofika yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!

Gade chapit la Kopi




Hosea 13:13
23 Referans Kwoze  

Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa, na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.


Kama vile mama mwenye mimba anayezaa analia na kugaagaa kwa uchungu, ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Yawe.


Lakini walipouona Sayuni, wakashangaa; wakashikwa na hofu na kukimbia.


Nao wakamwambia Isaya: “Hezekia anasema hivi: ‘Leo ni siku ya huzuni, ya kuazibiwa na ya kuzarauliwa. Sisi tumekuwa kama mwanamuke anayetaka kuzaa mutoto, lakini hana nguvu ya kumuzaa.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Mwenye akili anaona hatari na kujificha, lakini wajinga wanajitokeza mbele na kuumia.


Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu: “Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako. Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.” Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.


Lakini Paulo alipokuwa akihubiri juu ya haki, juu ya kujizuiza na juu ya siku ya hukumu ya Mungu itakayokuja, Feliki akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kujiendea. Nitakuita tena nitakapopata wakati.”


Watu wa Damasiki wamevunjika moyo; wamegeuka kusudi wapate kukimbia; hofu kubwa imewashika, uchungu na huzuni vimewapata, kama mwanamuke anayezaa.


Mujiulize sasa na kufahamu: Mwanaume anaweza kuzaa mutoto? Mbona basi, ninamwona kila mwanaume anajikamata kwenye kiuno kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa na nyuso zimebadilika?


Enyi wakaaji wote wa Lebanoni, ninyi munaokaa salama kati ya miti ya mierezi, mutaugua sana wakati mutakaposhikwa na uchungu unaokuwa kama wa mwanamuke anayezaa!


Utasema nini juu ya wale uliowazoeza kuwa warafiki zako, wale ambao wewe mwenyewe uliwafundisha, watakapokushinda na kukutawala? Si utashikwa na uchungu sawa vile mwanamuke anayezaa?


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Namna gani ninaweza kumufikisha mutoto kwa saa ya kuzaliwa, halafu nimuzuize asizaliwe? –Ni Yawe anayesema hivyo.– Au mimi mwenye kuwajalia watoto, namna gani nitafunga uzazi? –Ni Mungu wenu anayesema hivyo.


Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Munaweza namna gani kumulipa hivyo Yawe, enyi watu wapumbafu na wasiokuwa na akili? Yeye siye baba yenu aliyewaumba, aliyewafanya na kuwaimarisha?


Matendo yao yanawazuia wasimurudilie Mungu wao. Wamejaa uzinzi ndani ya mioyo yao; hawanijui mimi Yawe.


kwa sababu malaika wa Bwana alishuka mara kwa mara ndani ya kile kisima na kutikisa maji. Na mugonjwa wa kwanza aliyeingia ndani ya maji kisha kuyatikisa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite