Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Watu wa Efuraimu wananizunguka kwa uongo, na Waisraeli kwa udanganyifu. Lakini watu wa Yuda wanaendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu Mutakatifu.

Gade chapit la Kopi




Hosea 12:1
20 Referans Kwoze  

Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.


Umepandikizwa, lakini, utastawi? Upepo mukali wa mashariki unapovuma juu yake utanyauka; utakaukia palepale kwenye udongo ulikoota.


Waongozi wenu watapeperushwa na upepo, wapenzi wenu watapelekwa katika uhamisho. Halafu mutapata haya na kufazaika, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Mwenye hekima anajibu bila kufikiri na kujaa maneno ya burebure?


Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.


Halafu, nyuma ya hayo, masuke mengine saba membamba na yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa yakatokea.


Kwa nini unaniachilia hivi, ukibadilishabadilisha mwenendo wako? Utafezeheshwa na Misri kama ulivyofezeheshwa na Asuria.


Nitawafukuza ninyi mbali nami kama nilivyowatupilia mbali wandugu zenu, wote wa uzao wa Efuraimu.


Tumewanyooshea Wamisri na Waasuria mikono, kusudi tupate chakula cha kutosha.


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Efuraimu ni kama njiwa mujinga asiyekuwa na akili; mara yuko Misri, mara Asuria kwa kuomba musaada.


Tena alitengeneza pahali pa kuabudia miungu mingine katika milima ya Yuda na kusababisha wakaaji wa Yerusalema kukosa uaminifu na watu wa Yuda kupotoka.


Lakini walimudanganya kwa maneno yao; walimwambia uongo.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Nitaizuia hasira yangu kali; sitamwangamiza tena Efuraimu, maana mimi ni Mungu, wala si mwanadamu. Mimi ndimi Mutakatifu kati yenu, nami sitakuja kuwaangamiza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite