Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.

Gade chapit la Kopi




Hosea 11:1
18 Referans Kwoze  

Akakaa kule mpaka Herode alipokwisha kufa, kusudi yatimie maneno haya Bwana aliyosema kwa njia ya nabii: “Nilimwita mwana wangu arudie toka Misri.”


Nawe utamwambia mufalme wa Misri kwamba Yawe anasema hivi: ‘Israeli ni mwana wangu, muzaliwa wangu wa kwanza.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali, kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani, akajipamba kwa pete zake na ushanga, na kuwaendea wapenzi wake, akanisahau mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwenda uwatangazie waziwazi wakaaji wote wa Yerusalema na kusema hivi: Yawe anasema hivi: Ninakumbuka wema wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama muchumba wako. Ulinifuata katika jangwa kwenye inchi ambayo haikupandwa kitu.


Yawe anasema hivi: Nimewapenda ninyi siku zote. Lakini ninyi wazao wa Yakobo munaniuliza: Umetupenda namna gani? Yawe anasema hivi: Si Esau alikuwa ndugu wa Yakobo? Hata hivyo nilimupenda Yakobo


Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.


Mimi nilipopita karibu nawe, nikakuona ukigaagaa katika damu yako, nikakuambia:


“Yawe hakuwapenda ninyi na kuwachagua kwa sababu ninyi ni wengi sana kuliko watu wengine; ninyi mulikuwa wachache kuliko mataifa mengine katika dunia.


Efuraimu amesema: Mimi ni tajiri! Mimi nimejitajirisha! Sikufanya mabaya kwa kupata hii faida.


Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”


Wimbo wa safari za kidini. Kila mutu katika Israeli aseme: “Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu”.


Yawe anasema hivi: Nimeiacha nyumba yangu; nimeitupa mali yangu mimi mwenyewe. Israeli, mupenzi wangu wa moyo, nimemutoa katika mikono ya waadui zake.


Ndivyo itakavyokuwa kwenu enyi watu wa Beteli, kwa sababu ya uovu wenu mukubwa. Kutakapopambazuka mufalme wa Israeli atauawa.


‘Ninyi wenyewe mumeona jinsi nilivyowatendea Wamisri na jinsi nilivyowapeleka ninyi kama vile tai anavyopeleka watoto wake kwa mabawa, nikawaleta kwangu.


Yawe anawapenda watu wake, anawalinda watakatifu wake wote. Wanamufuata na kupata maagizo kutoka kwake.


Ninyi ni wa bei kali mbele yangu, ninawaheshimu na kuwapenda. Kwa hiyo, ninatoa watu kusudi niwapate ninyi, ninayaachilia mataifa pahali pa maisha yenu.


Katika machukizo yako yote pamoja na uzinzi wako haukuzikumbuka siku za utoto wako, wakati ulipokuwa uchi kabisa, bila kitu, ukigaagaa katika damu yako!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite