Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.

Gade chapit la Kopi




Hosea 10:5
20 Referans Kwoze  

Utukufu wa Efuraimu utatoweka kama ndege; watoto hawatazaliwa tena, hakutakuwa watoto wa kuzaliwa, wala hakutakuwa atakayepata mimba!


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Kisha akawaondoa makuhani wote waliobarikiwa na wafalme wa Yuda kwa kufukiza ubani katika pahali pa kuabudia katika miji ya Yuda na kunzunguka Yerusalema, vilevile wale waliofukiza ubani kwa Bali, jua, mwezi, nyota na jeshi la mbingu katika nyumba ya Yawe.


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Hivi kunakuwa hatari, na si kwa kazi hii yetu kuzarauliwa tu, lakini vilevile hekalu la mungu mukubwa muke, Artemi, litahesabiwa kuwa kitu bure. Na tena utukufu wake utapunguka, yeye anayeabudiwa na watu wote wa Azia na dunia nzima!”


Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuazibu inchi ya Yuda, pamoja na wakaaji wote wa Yerusalema. Nitaangamiza mabaki yote ya mungu Bali kutoka inchi hii, na hakuna atakayetambua jina lao.


Yeroboamu akajichagulia makuhani wake mwenyewe wa kutumika kwenye nafasi za ibada za miungu na wa kuabudu mizimu na sanamu za wana-ngombe alizojitengenezea.


Walivunja amri zote za Yawe, Mungu wao. Wakatengeneza sanamu za miungu ya wana-ngombe wawili wa madini yenye kuyeyushwa, wakatengeneza sanamu za Ashera, wakaabudu jeshi la mbingu, na wakamutumikia Bali.


Lakini hakuacha zambi zile za Yeroboamu mwana wa Nebati ambaye aliwasukuma Waisraeli watende zambi, ni kusema ile ibada ya sanamu za wana-ngombe wa zahabu kule Beteli na Dani.


Mika akasema: “Ninyi mumebeba miungu yangu niliyojitengenezea, mukamutwaa na kuhani wangu, mukaniacha bila kitu chochote. Munaweza namna gani basi kuniuliza nina shida gani?”


Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.


“Sasa ninyi munazani munaweza kupinga ufalme wa Yawe ambao Daudi na wazao wake walipewa kwa sababu muko na jeshi kubwa na sanamu za zahabu za wana-ngombe, Yeroboamu alizowatengenezea kuwa miungu yenu!


Wanajiinamisha, wanainama pamoja. Hawakuweza kuziokoa sanamu zao. Wao wenyewe vilevile wamepelekwa katika utumwa!


Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.


Siku nitakapowaazibu Waisraeli kwa sababu ya makosa yao, nitayaharibu vilevile mazabahu ya muji wa Beteli. Nitazikata pembe za kila mazabahu na kuziangusha chini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite