Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 10:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mioyo yao imejaa udanganyifu. Sasa ni lazima wabebe makosa yao. Yawe atabomoa mazabahu zao na kuziharibu nguzo zao.

Gade chapit la Kopi




Hosea 10:2
24 Referans Kwoze  

Nitaziongoa sanamu za Ashera kutoka kwenu, na kuiangamiza miji yenu.


Kisha, Elia akawakaribia watu hao, akawaambia: “Mutaendelea kusitasita ndani ya mioyo mpaka wakati gani? Ikiwa Yawe ni Mungu, mumufuate; lakini ikiwa Bali ni Mungu, basi, mumufuate.” Lakini watu hawakumujibu neno lolote.


Ninyi watu wasiokuwa na uaminifu! Hamujui kwamba kupenda raha ya dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi yeye anayetaka kupenda raha za dunia anajifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu.


kwa sababu ni mutu wa nia mbili, na mwenye kugeukageuka katika mwenendo wake.


Nitawaangamiza wote wanaoinama juu ya dari, wakiabudu jeshi la mbinguni. Nitawaangamiza wale wanaoniabudu na kuapa kwa jina langu, tena wanaapa vilevile kwa jina la mungu Milkomu.


“Hakuna mutumishi anayeweza kutumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kumutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.”


“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Efuraimu amechanganika na watu wa mataifa. Anaonekana kama mukate ambao haukugeuzwa.


Ataivunja minara ya mungu wao inayokuwa huko Heliopoli katika inchi ya Misri, na atateketeza mahekalu ya miungu ya Misri kwa moto.


Watu hao hawajui wala hawaelewi kitu chochote. Wamefungwa macho wasipate kuona na akili wasipate kufahamu.


Lakini, kesho yake asubui walipoamuka, waliona kwamba sanamu ya Dagoni imeanguka uso chini mbele ya Sanduku la Yawe, kichwa, miguu na mikono ya sanamu hiyo, vyote vilikuwa vimekatika, vikakuwa vimelala chini kwenye kizingiti cha mulango. Kiwiliwili cha sanamu ya Dagoni ndicho tu kilikuwa kimebakia.


Musipende dunia, wala mambo yanayokuwa katika dunia. Mutu akipenda dunia, hawezi kumupenda Mungu Baba.


Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.


Mimi niliongea na manabii; ni mimi niliyewapa maono mengi, na kwa njia yao nilitangaza mupango wangu.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.


Mimi Yawe nitaigusa mioyo ya Waisraeli kusudi wanirudilie, maana wamejitenga mbali nami kwa kuabudu sanamu zao za miungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite