Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 10:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Ndivyo itakavyokuwa kwenu enyi watu wa Beteli, kwa sababu ya uovu wenu mukubwa. Kutakapopambazuka mufalme wa Israeli atauawa.

Gade chapit la Kopi




Hosea 10:15
8 Referans Kwoze  

Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Mufalme wa Samaria atapelekwa, kama kipande cha muti juu ya maji.


Basi ni kusema kile kinachokuwa kizuri kimeniletea kifo? Hapana hata kidogo! Ni zambi ndiyo iliyoniletea kifo. Lakini kusudi zambi ionekane kuwa zambi kweli kweli, ilipitia kwa njia ya kile kinachokuwa kizuri kwa kusababisha kifo changu. Hivi kwa njia ya amri ile, zambi ilizidi kujikamilisha kuwa zambi kabisa.


Wakati huo watasema: Hatuna tena mufalme, kwa maana hatumwogopi Yawe; lakini, naye mufalme atatufanyia nini?


Lakini sasa Yawe anasema hivi: Nyuma ya miaka mitatu kamili, ikihesabiwa kama vile mutumishi anavyohesabu siku zake, utukufu wa Moabu utapunguka. Ingawa watu wake ni wengi, watakaobaki wazima watakuwa wachache na wazaifu.


Kwa hiyo fujo ya vita itawafikia watu wako, kuta zako zote zitaharibiwa. Kama vile mufalme Salmani alivyoharibu Beti-Arbeli katika vita, wamama wakapondwa pamoja na watoto wao.


Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite