Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 10:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Lakini ninyi mumepanda uovu, ninyi mumevuna ubaya; mumekula matunda ya uongo wenu. Wewe Israeli ulitegemea nguvu zako mwenyewe, na wingi wa waaskari wako.

Gade chapit la Kopi




Hosea 10:13
19 Referans Kwoze  

Mimi nimeona kwamba wanaopanda uovu na ubaya wanavuna yaleyale.


Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


Anayepanda ubaya atavuna hasara. Uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.


Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.


Mufalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na kundi kubwa; wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele, atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako; atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.


Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu; wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.


Tena, nimeona kitu kimoja hapa chini ya jua, kwamba wenye kukimbia mbio hawashindi katika mashindano ya kukimbia, wala wenye nguvu hawashindi vita, wenye hekima hawapati chakula, wenye akili hawatajiriki, wala wenye ujuzi hawapandi vyeo. Lakini wakati wa bahati unawapata wote pamoja.


Mushuhuda mwongo hatakosa kuazibiwa; anayesema uongo hataepuka azabu.


Ukweli unadumu milele, lakini uongo ni wa muda kidogo tu.


Mutu muzuri anapata uzuri kutokana na maneno yake, lakini mudanganyifu anaishi kwa kutesa kwa ukali.


hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Wanajishibisha kwa sadaka za watu wangu wenye zambi. Wana hamu sana ya kuwaona wakitenda zambi.


Kumbuka mezali ya kale inayosema ‘Uovu unatoka ndani ya mwovu’, lakini sitanyoosha mukono juu yako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite