Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 10:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nitawaendea watu hawa wapotovu na kuwaazibu; watu wa mataifa watakusanyika kwa kuwashambulia, watakapoazibiwa kwa ajili ya zambi zao nyingi.

Gade chapit la Kopi




Hosea 10:10
20 Referans Kwoze  

Ndivyo nitakavyomaliza hasira yangu, nami nitakuwa nimetuliza kasirani yangu na kufarijika ndani ya moyo. Hapo ndipo watakapojua kwamba mimi, Yawe, nimewaazibu kwa sababu ya wivu wangu kwa ukosefu wenu wa uaminifu.


Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani; nitawaazibu kwa sababu ya mwenendo wao, nitawalipiza matendo yao wenyewe.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.


Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa, lakini mimi nitawakusanya. Na hapo watasikia uzito wa muzigo wa mufalme wa wakubwa.


Mupige baragumu! Adui anakuja kama tai kuishambulia nyumba ya Yawe, kwa sababu wamelivunja agano langu na kuiasi sheria yangu.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kundi la watu litaletwa, litawatisha na kuwanyanganya mali zao.


Kwa hiyo nikamutoa katika mikono ya Waasuria wapenzi wake, ambao aliwatamani sana.


Hivi, kasirani yangu itatosheka juu yako, wivu niliokuwa nao juu yako utakwisha; nitatulia wala sitaona hasira tena.


Basi, mimi nitawakusanya wapenzi wako wote uliojifurahisha nao, wote uliowapenda na wote uliowachukia. Nitawakusanya toka pande zote wakushambulie. Nitawafunulia uchi wako wapate kuuona.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Zedekia, nitakugeuzia wewe mwenyewe silaha unazozitumia kwa kupigana na mufalme wa Babeli na waaskari wake wanaozunguka inje ya kuta za muji wenu. Nitazikusanya silaha zile katikati ya muji huu.


Ninyi mumenikataa mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ninyi mumeniacha na kurudi nyuma. Kwa hiyo nimenyoosha mukono kwa kuwaangamiza. Nimechoka na kuwahurumia.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.


Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


Unaweza kumufunga mbogo kamba kwa kulima shamba, au akokote jembe la kulima?


Basi, zoruba itawapeperusha, nao watapata haya kwa ajili ya sadaka zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite