Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hosea 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Yezereheli”, maana kisha siku chache tu, nitaiazibu jamaa ya Yehu kwa mauaji aliyofanya katika bonde la Yezereheli. Hivi nitavunja ufalme katika taifa la Israeli.

Gade chapit la Kopi




Hosea 1:4
32 Referans Kwoze  

Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.


Gomeri alipata mimba tena, akazaa mutoto mwanamuke. Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Asiyehurumiwa”, maana sitawahurumia tena Waisraeli wala sitawasamehe.


Kwa sababu ulifuata njia ya dada yako, basi, mimi nitakupa kikombe kilekile cha azabu ukikunywe.


Hao walimuvua nguo zake na kumwacha uchi. Waliwakamata watoto wake, naye mwenyewe wakamwua kwa upanga. Azabu hiyo aliyopata ikakuwa fundisho kwa wanawake wengine.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi juu ya wachungaji wanaowachunga watu wangu: Ninyi munasambaza kondoo wangu na kuwafukuza, wala hamukuwatunza. Basi, nami vilevile nitawaazibu kwa ajili ya matendo yenu maovu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


Walipofika Samaria, Yehu aliua jamaa yote ya Ahabu bila kumwacha hata mumoja wao, sawa vile Yawe alivyomwambia Elia itakavyokuwa.


Kisha akamupeleka Simoni kwa Yesu. Yesu akamwangalia, akasema: “Wewe ndiwe Simoni mwana wa Yoane, sasa utaitwa Kefa.” (Jina “Kefa” ni sawasawa na “Petro” na maana yake ni “Jiwe.”)


Zakaria akaomba wamuletee kibao, naye akaandika maneno haya juu yake: “Jina lake ni Yoane.” Wote wakashangaa.


Utapata mimba, utazaa mutoto mwanaume, na utamwita jina lake Yesu.


Lakini yule malaika akamwambia: “Zakaria, usiogope, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Muke wako Elizabeti atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yoane.


Yeye atazaa mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yesu, kwa maana ndiye atakayewaokoa watu wake toka katika zambi zao.”


Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.


Kweli, nitakuoa kwa uaminifu, nawe utanijua mimi Yawe.


Nitakomesha furaha zake zote, sikukuu zake za mwandamo wa mwezi na za Sabato, na sikukuu zote zilizoamriwa.


Katika mwaka wa makumi tatu na nane wa utawala wa Azaria mufalme wa Yuda, Zakaria mwana wa Yeroboamu akaanza kutawala Israeli. Akatawala kwa muda wa miezi sita.


Kesho yake asubui, Pashuri akamufungua Yeremia toka minyororo ile. Yeremia akamwambia hivi: Yawe hakuiti tena jina lako “Pashuri”, lakini “Kitisho Kila Pahali”.


Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya: Yezereheli, Kesuloti, Sunemu, Hafaraimu, Sioni, Anaharati, Rabiti, Kisioni, Ebesi, Remeti, Eni-Ganimu, Eni-Hada na Beti-Pasesi. Vilevile, mupaka wao ulifika Tabori, Sahasuma, Beti-Semesi na kuishia kwenye muto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.


Katika muji wa Samaria kulikuwa wana makumi saba wa Ahabu. Yehu akaandika barua na kutuma barua kwa watawala wa muji, kwa viongozi na kwa walinzi wa wana wa Ahabu. Barua yenyewe ilisema hivi:


Nikalala na muke wangu ambaye vilevile ni nabii, akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Yawe akaniambia: Umupe mutoto huyo jina “Teka-haraka-nyanganya-upesi.”


Ninauangalia ufalme wenye zambi, na nitauangamiza kabisa kutoka katika dunia. Lakini sitawaangamiza wazao wote wa Yakobo. –Ni ujumbe wa Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite