Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Hesabu 9:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Lakini mutu yeyote ambaye ni safi au hayuko katika safari asipofanya sikukuu ya Pasaka, atatengwa na watu wake kwa kuwa hakunitolea sadaka kwa wakati uliopangwa. Mutu huyo atabeba lazima ya zambi yake.

Gade chapit la Kopi




Hesabu 9:13
24 Referans Kwoze  

Yawe akaendelea kusema: “Kwa muda wa siku saba, mutakula mikate isiyotiwa chachu. Siku ya kwanza ya siku hizo saba, mutaondoa chachu katika nyumba zenu. Mutu yeyote akikula kitu kilichotiwa chachu katika muda ule wa siku saba, anapaswa kuondolewa kati ya Waisraeli.


Mwanaume yeyote asiyetahiriwa atatengwa na watu, maana atakuwa amevunja agano langu.”


wakawaambia: Sisi tuko wachafu kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tukatazwe kumutolea Yawe sadaka zake kwa wakati uliopangwa pamoja na Waisraeli wengine?


Basi muangalie vizuri kusudi musikatae kumusikiliza yule anayesema nanyi. Wale waliokataa kusikiliza yule aliyewaonya hapa katika dunia hawakuponyoka azabu ya Mungu. Si jambo hilo linaonyesha wazi kwamba sisi hatutaweza kuponyoka kama tunamugeuzia mugongo yule anayetutolea maonyo kutoka mbinguni?


Hivi vilevile Kristo naye alijitoa kufa mara moja kusudi aondoe zambi za watu wengi. Naye atarudi tena, si kwa ajili ya kuondoa zambi, lakini kwa kuwaokoa wale wanaomungojea.


kisha wakianguka, haiwezekani kuwarudisha hata wapate kugeuka mara ingine toka katika matendo yao mabaya. Kwa sababu wamemutundika wao wenyewe Mwana wa Mungu mara ya pili na kumupatisha haya mbele ya watu.


Basi, namna gani sisi tutaponyoka azabu kama hatushuguliki na wokovu mukubwa kama huu? Ni Bwana mwenyewe aliyetangaza kwanza habari za wokovu huu, na wale waliomusikia walihakikisha kwetu kwamba ni za kweli.


Na ninyi Ohola na Oholiba, mutaazibiwa kutokana na uzinzi wenu na zambi yenu ya kuziabudu sanamu za miungu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Bwana wenu Yawe.


Anayegusa maiti, ni kusema mwili wa mutu aliyekufa, asipojitakasa, anachafua hema la Yawe, naye atatengwa na watu wa Israeli. Mutu huyo atabaki muchafu kwa sababu hakunyunyiziwa yale maji ya utakaso.


Mume wake hatakuwa na kosa lolote, lakini mwanamuke atabeba lazima ya uovu wake.


Kama mutu akilala na muke wa baba yake, mukubwa au mudogo, anamupatisha baba yake mukubwa au mudogo haya. Wote wawili watabeba lazima ya zambi yao. Wote wawili watakufa bila watoto.


Kama mutu yeyote wa jamii ya Israeli au mugeni anayeishi kati yao anakula damu yoyote, mimi nitamukasirikia mutu yule aliyekula damu na kumutenga mbali na watu wake.


bila kumuleta nyama huyo kwenye mulango wa hema la mukutano kwa kumutolea Yawe mbele ya makao yake, mutu yule atakuwa na kosa ya kumwanga damu. Amemwanga damu na atatengwa na watu wake.


Kwa hiyo, makuhani washike agizo langu, kusudi wasifanye zambi na kuuawa. Mimi Yawe ndiye ninayewatakasa.


Katika siku hizo saba, musikuwe na chachu yoyote katika nyumba zenu. Mutu yeyote, akuwe mugeni au mwenyeji, akikula kitu kilichotiwa chachu, ataondolewa katika kusanyiko la Waisraeli.


Waisraeli wote pamoja watashika sikukuu hiyo.


Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumupakaa mutu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mutu huyu atatengwa mbali na watu wake.


Yeyote atakayejitengenezea ubani wa aina hiyo na kuutumia kama manukato yake pekee, atatengwa mbali na watu wake.


Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote atakayemulaani Mungu wake atabeba lazima ya zambi yake.


Lakini mutu muchafu asipojitakasa, mutu huyo atatengwa mbali na jamii, kwa sababu anachafua hema la Yawe. Kwa vile hakunyunyiziwa maji ya utakaso, yuko muchafu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite